Wananchi wilayani Bunda walalamika Kiongozi kuchukuwa mali zao kwa kosa la kutokuhudhuria shughuli za maendeleo - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Saturday 24 February 2018

Wananchi wilayani Bunda walalamika Kiongozi kuchukuwa mali zao kwa kosa la kutokuhudhuria shughuli za maendeleo

Zaidi ya wananchi 20  kutoka katika kitongoji cha Nyamigunga kijiji cha Ligamba B kata ya Sazira wilayani Bunda Mkoani Mara wameoongozana kimakundi  na kufika  katika ofisi za redio mazingira na kutoa malalamiko yao dhidi ya mtendaji wao kufanya msako kuharibu,kuvunja milango  na kuchukua mali zao kwa nguvu.

Wameeleza kuwa mtendaji huyo ameendesha msako huo kwa madai ya kuwa wananchi ho wameshindwa kushiriki maendeleo ya ujenzi wa shule ya msingi unaoendelea kijijini hapo .

Mashaka Charles mkazai wa kitongoji hicho amesema kuwa  hakuwa nyumba ni na wakati amerudi amekuta mtendaji huyo amechukua sola yake kwa madai ya kutohudhuria maendeleo licha ya kutokuwa na taarifa ya uwepo wa kushiriki maendeleo hayo kwa siku hiyo.

Ameongeza kuwa pamoja na kufanyiwa kitendo hicho lakini mtendaji huyo amekuwa mungu mtu kwani amekuwa akitisha kuwafunga watu pindi anaposhauriwa.

Naye Gaudensia Philipo mkazi wa kitongoji hicho amesema mtendaji alipofika kwake amevunja mlango na kuchukua mbuzi,baada ya kumuuliza kwanini anafanya hivyo mtendaji akamweleza kwanini hawaendi kwenye maendeleo.

Amesema licha ya kupokonywa mbuzi wake kwa kutoshiriki maendeleo awali aliruhusiwa kutokwenda maendeleo kutokana na ujauzito alionao.

Majura Apolinary  pamoja na Majige Gerad ambao pia ni wananchi wa kitongoji cha Nyamigunga waliochukuliwa 'solar' suala hilo hawajapendezwa nalo na wanafanyiwa unyanyasaji hivyo wanaiomba serikali iwasaidie.
Aidha mwenyekiti wa kitongoji hicho Bwana KASALU KISHOSHA ameeleza kwamba jambo hilo limetokea katika kitongoji chake na kwa familia zinazokadiriwa kufikia 70 licha ya wachache tu ndio walioamua kwenda polisi.
Amesema kama mwenyekiti wa eneo husika alimshauri mtendaji huyo kutotumia utaratibu huo wa kuchukua maamuzi ya kuvunja milango na kuchukua mali za wananchi wakiwa hawapo katika kaya zao.

Modestusa Chama ni mtendaji wa kata ya Nyamag’uta jirani na kata ya Sazira amefafanua suala hilo kama ukiukwaji wa utaratibu kwani kwa mujibu wa sheria mtu anaegoma kushiriki maendeleo anatakiwa kuandikiwa  samas ya kuitwa mahakamani ili akahojiwe ni kwanini asichukuliwe hatua kwa kukwamisha maendeleo.
Hata hivyo kwa upande wa Mtendaji wa kijiji hicho bwana  Jonson Charles amekiri kufanyika kwa msako huo, ambapo ameeleza kuwa wamezingatia utaratibu uliowekwa na wananchi wenyewe katika mkutano wa wananchi kupitia sheria ndogo walizojiwekea ya kukamata mali pindi mtu anaposhindwa kushiriki maendeleo bila taarifa.
Amesema jumla ya kaya 35 zilifikiwa na msako huo ambapo,baada ya hutua hiyo wananchi walienda polisi lakini wakashauriwa waende wakae pamoja na uongozi kamaliza tatizo hilo.
Ameongeza kuwa makubaliano walioweka ni mwananchi kukomboa mali zake kwa kutoa shilingi elfu tano na mpaka sasa tayari wameshajitokeza waliofanya hivy na jumla ya shilingi laki moja imepatikana-100,000/-.
Naye Diwani wa kata ya Sazira Bwana Jumanne Mnyaruga amedai kuwa wananchi hao kukimbilia vyombo vya habari na polisi siyo suluhisho badala yake wanapaswa kukaa na uongozi wao ili kupata muafaka.

No comments:

Post a Comment