Wamiliki wa vyombo vya habari nchini wametakiwa kutoingilia
uhuru wa wanahabari katika vituo vyao kwasababu vinaongozwa na sera na misingi yataaluma
yahabari.
Hayo yamebainishwa mjini DODOMA na Mkufunzi Mwandamizi
wa Radio za kijamii Bi Rose Mwalimu katika warsha yakuwajengea uwezo waandishi
wa habari vijijini inayowakutanisha wadau wa redio za jamii nchini.
Amesema ni vyema wanahabari wakawa huru katika kutimiza
wajibu wao kitaaluma ili kuihudumia jamii na kujiepusha na
masuala binafsi.
Warsha hiyo ya siku nane inayo washirikisha wadau
wa radio zajamii 24 imeandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu,
Sayansi na Utamaduni, UNESCO ili kuwajengea uwezo waandishi wa habari kujiendesha
kwakujiamini.
No comments:
Post a Comment