Bunda kuna jumla ya vikundi 31 vya ulinzi shirikishi ambavyo vipo hai na katika maeneo hayo matukio ya uharifu yamepungua kwa kiasi kikubwa.
Na Adelinus Banenwa
Imeelezwa kuwa sehemu zenye vikundi vya ulinzi shirikishi yaani polisi jamii wilayani Bunda matukio ya kiharifu yamepungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na maeneo ambayo hakuna kabisa vikundi hivyo.
Hayo yamesemwa na mkaguzi wa polisi Jonas Kaijage ambaye ni mratibu wa polisi jamii wilayani Bunda kupitia kipindi cha Asubuhi leo kinachorushwa Radio Mazingira fm ambapo amesema kwa wilaya ya Bunda kuna jumla ya vikundi 31 vya ulinzi shirikishi ambavyo vipo hai na katika maeneo hayo matukio ya uharifu yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Kaijage ameongeza kuwa sheria ya kuwepo kwa ulinzi shirikishi una lengo la kuishirikisha jamii katika masuala ya ulinzi na usalama katika maeneo yao ndiyo maana kama jeshi la polisi wanahusika kutoa elimu na maelekezo kwa vikundi vinavyoanzishwa.
Kaijage ametoa wito kwa jamii kuhakikisha kupitia kwa wenyeviti wa mitaa, vijiji na vitongoji wanaanzisha vikundi hivyo ili kuweka usalama kwenye maeneo yao kwa kuwa sasa jeshi la polisi limesogeza karibu kabisa huduma na vikundi hivyo ikiwa nipamoja na kila kata kuwepo kwa polisi kata ambaye anasaidia kutoa elimu kwa vikundi hivyo.
Kwa upande mwingine Insp Kaijage amewataka wafanyabiashara wanaotoa huduma za kifedha kwa maana ya huduma pesa kuwa waangalifu kutokana na changamoto za wizi na utapeli ambao unaonekana kushamili kwa siku za hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment