Showing posts with label COMMUNITY. Show all posts
Showing posts with label COMMUNITY. Show all posts

Wednesday, 26 February 2025

 

Wazazi Sazira na Sizaki Sec wapewa tano kwa wanafunzi wote kupata chakula shuleni

26 February 2025, 

Katika picha akionekana Mhe Robert Chacha Maboto mbunge jimbo la Bunda mjini katika shule tofauti alizozitembelea.

Mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Chacha Maboto amewapongeza wazazi na waleza wa shule za sekondari za Sazira na Sizaki kwa kuchanga chakula cha wanafunzi shuleni.

Na Adelinus Banenwa

Mbunge wa jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Chacha Maboto amewapongeza wazazi na waleza wa shule za sekondari za Sazira na Sizaki kwa kuchanga chakula cha wanafunzi shuleni na kufanya wanafunzi wote kupata chakula.

Mhe Mbunge ametoa shukra hizo katika ziara yake ikiwa ni siku ya pili ya ziara hiyo yenye lengo la kuhamasisha uchangiaji wa chakula cha wanafunzi mashuleni ili kuongeza ufaulu.

Wanafunzi shule ya sekondari Sizaki wakionesha furaha baada ya kupokea chakula kutoka kwa Mbunge jimbo la Bunda mjini Mhe Robert Chacha Maboto

Mhe Maboto amesema ili mwanafunzi aweze kupata ufaulu mzuri ni lazima mzazi na serikali pamoja na walimu kila mmoja kutimiza wajibu wake ambapo kazi kubwa ya mzazi ni kununua vifaa vya shule na kuchangia chakula shuleni tu.

Amewataka wazazi wa maeneo mengine ndani ya jimbo la Bunda mjini kuiga mifano na mbinu wanazozitumia wazazi wa sazira na sizaki ili kuhakikisha watoto wote wanapata chakula.

Naye mkuu washule ya sekondari ya Sizaki mwalimu Maeda amesema mbinu pekee wanayoitumia kuhamasisha wazazi ni kuwaeleza umuhimu wa chakula kwa wanafunzi pia upatikanaji wa chakula kwa wanafunzi wote umewezesha kupata ufaulu kati ya daraja la 1 ha 4 na kufuta daraja 0

Nao wanafunzi katika shule alizozitembelea Mhe mbunge wamemshukuru huku wakiahidi kuendelea kuwahimiza wazazi waendelee kuchangia chakula muda wote.

Katika siku ya pili ya ziara yake Mhe mbunge Robert Maboto amezitembelea shule za sekondari za Bunda stoo, Migungani, Rubana, Kunzugu, Paul Jones, sizaki na shule ya Sekondari ya Sazira

Sunday, 16 February 2025

 

Wagonjwa 1,520 wahudumiwa bure katika kambi ya macho Bunda

16 February 2025, 

rais wa Chama cha Lions Clubs International, Mahamoud Rajuan,

Zaidi ya Wagonjwa 1,520 Wahudumiwa Bure Katika Kambi ya Matibabu ya Macho Bunda Manyamanyama.

Na Adelinus Banenwa

Zaidi ya wagonjwa 1,520 wa macho wamehudumiwa ndani ya siku mbili kati ya tatu katika kambi maalumu ya matibabu ya macho iliyofanyika katika Hospitali ya Bunda Manyamanyama.

Akizungumza katika kambi hiyo, rais wa Chama cha Lions Clubs International, Mahamoud Rajuan, amesema kati ya wagonjwa hao, 150 wamefanyiwa upasuaji wa macho kutokana na changamoto mbalimbali walizokuwa nazo, ikiwa ni pamoja na mtoto wa jicho.

Baadhi ya wagonjwa waliopata huduma katika kambi ya macho ikiwemo kufanyiwa upasuaji

Mahamoud amewashukuru wananchi kwa kujitokeza na pia kuwashukuru wafadhili waliowezesha kufanyika kwa kambi hiyo, ambapo huduma zilikuwa bure.

Sauti ya rais wa Chama cha Lions Clubs International, Mahamoud Rajuan,
Dr. Majey Majey, mganga anayehusika na huduma za matibabu ya macho

Naye, Dr. Majey Majey, mganga anayehusika na huduma za matibabu ya macho na vipimo, amesema kwa siku hizo mbili wamewahudumia wagonjwa 1,520 na wanashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kupata matibabu.

Dr. Majey ameeleza kuwa matatizo ya macho yanaweza kusababishwa na changamoto mbalimbali, ikiwemo aleji, mtoto wa jicho, presha ya macho, vumbi, moshi, na mengine, na hivyo wanatoa ushauri kulingana na chanzo cha ugonjwa wa kila mgonjwa.

Sauti ya Dr. Majey Majey, mganga anayehusika na huduma za matibabu ya macho
Baadhi ya wagonjwa waliopata huduma katika kambi ya macho ikiwemo kufanyiwa upasuaji

Kwa upande wao, baadhi ya wagonjwa waliopata huduma katika kambi ya siku tatu wamewashukuru kwa huduma walizopata, kwani hawakudaiwa fedha yoyote kuanzia kwenye vipimo hadi upasuaji.

Kambi hiyo ya matibabu ya macho katika Hospitali ya Bunda Manyamanyama ilianza tarehe 14 Februari na kumalizika leo, tarehe 16 Februari 2025, huku matibabu yaliyotolewa ikiwa ni pamoja na huduma za vipimo, ugawaji wa miwani ya jua na kusomea, pamoja na upasuaji, yote hayo yakitolewa bure.

Friday, 26 January 2018

Hatua za haraka zaanza kuchukuliwa kuondoa adha ya ukosefu wa choo Shule ya Bunda




Wanafunzi,Waalimu pamoja na wakazi wanaofanya shughuli zao katika shule ya Msingi Bunda halmashauri ya mji wa Bunda Mkoani Mara wako hatarini kupatwa na Magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu kutokana na shule hiyo kukosa choo jambo linalowalazimu wanafunzi pamoja na walimu kujisaidia mlimani.

Taarifa zinaeleza kwamba wanafunzi wa darasa la awali yaani chekechea,la kwanza, la pili na hata madarasa mengine baadhi yao hulazimika kuchimba mchanga kwa mikono katika eneo la uwanja wa mpira wa miguu shuleni hapo kisha hujisaidia haja kubwa na baadae huyafunika.

Alipoulizwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji huo Janeth Mayanja amesema kuwa suala hilo la ukosefu analitambua na tayari wameanza kulishughulikia kwa kujenga choo cha dharura kwa wanafunzi hao ikiwa sambamba na ujenzi wa matundu 16 ya vyoo vya kudumu.

Taarifa kutoka katika shule hiyo zinadai kwamba leo wameanza uchimbaji wa matundu hayo ya vyoo.

Hata hivyo wananchi wameshukuru redio mazingira fm  pamoja na serikali ya mji wa bunda chini ya mkurugenzi wake Janeth Mayanja  kwa hatua alizozichukua katika kunusuru adha hiyo .

Thursday, 25 January 2018

Mkurungezi wa mamlaka ya Maji Bunda BUWASA asimamishwa kazi kupisha uchunguzi dhidi tuhuma zinazomkabili



Imeelezwa kuwa Mkurungezi wa Mamlaka ya maji Bunda BUWASA bwana Mansur Mandemula amesimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi kufuatia tuhumu zinazomkabili za kuwa na duka la vifaa vya huduma ya maji jambo ambalo ni kinyume.

Akizungumza na radio mazingira fm Kwanjia ya simu Mkuu wa Wilaya Ya Bunda Mwl.Lydia Bupilipili amethibitisha kusimamishwa kwa mkurungezi huyo na kwamba siku ya leo ndiyo amekabidhi ofisi ili kupisha uchunguzi.

Bipilipili amesema tayari bodi ya maji Imevunjwa kutokana na kuwepo kwa taarifa za kumtetea Mkurungezi huyo huku wakishindwa kutimiza wajibu wao kama bodi na badala yake wamesababisha hadi deni limefika milioni mia nne sabini na saba paka sasa hivi.

Aidha Bupilipili amesema kuwa awali aliwaeleza wajumbe wa bodi hiyo kuwa wao wapo kwajili ya wananchi na sio watu wengine na kwamba bodi ilionekana kutokuwa wabunifu katika kazi zao kwa wananchi.

Katika hatua nyingine Bupilipili amesema moja ya agizo la waziri mkuu ni kutuma wataalam kutoka Makao makuu TAMISEMI ili kuja kuchunguza miradi yote ya maji katika Wilaya ya Bunda ambapo tayari wataalam hao wameshafika na tayari wameshaanza kazi kama maagizo yalivyokuwa.

Sunday, 21 January 2018

Mwalimu wa Shule ya Msingi Bigutu adakwa na wananchi baada ya kukutwa akiiba vifaa vya ujenzi shuleni Mjini Bunda


 
Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Bigutu katika kata ya Bunda stoo hamashauri ya mji wa Bunda aliyejulikana kwa majina ya Said  MNEMA amekamatwa na wananchi kwa tuhuma za kukutwa Akiiba vifaa vya ujenzi wa shule hiyo vilivyochangwa kwa fedha za Wananchi.


Pendo Maguya ni mwananchi wa kata hiyo aliyeshuhudia mwalimu huyo akiiba sementi hatiamye kutoa taarifa kwa aliyekuwa mwenyekiti wa kitongoji hicho.

Amesema yeye pamoja na mwenzake Anastazia malagira walihisi kuwepo kwa uwizi katika vifaa hivyo vya ujenzi baada ya kuona mtu mmoja ambaye hawakumtaja jina mwenye toroli akisomba saruji kupeleka kwa mwalimu huyo.

Aidha Anastazi Malagira amesema ameshuhudia wizi wa sementi mifuko minne,Nondo na misumari,ambapo ameongeza kuwa walikuwa wanatoka kufata maji ndipo wakaona pikipiki na mtu mwenyetoroli akisimama katika mlango wa ofisi ya mwalimu mkuu na wakaamua kusubiri kuona kinachotoka ndani ya ofisi hiyo na kushuhudaia watu hao wakitoa vifa hivyo.

Naye kwa upande wake Makam mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo ameeleza kwamba amepata taarifa za wizi huo na kufika shuleni hapo ambapo alimkuta aliyekuwa mwenyekiti wa mtaa huo akiwa na mwalimu mkuu na alipomhoji mtuhumiwa huyoa alimweleza kuwa wakae wayamalize.
Hata hivyo Kaimu Afisa elimu wa shule ya msingi halmashauri ya mji huo Hundi Tanga Amesema kuwa amepata taarifa za tukio hilo na kuchukua hatua za kutoa taarifa polisi.

Diwani wa kata hiyo Chiruma Daud Subi ameeleza kwa amepata taarifa hizo na kufika katika eneo la tukio ambapo ameongeza kwamba baada ya ufuatiliaji wameshuudia matofari zaidi ya 300 pia zimehamishwa shuleni hapo na kupelekwa eneo analojenga mwalimu huyo anaetuhumiwa kwa wizi huo.

Hata hivyo Mkurugenzi wa mji wa Bunda Janeth Mayanja amelaani vikali tabia hiyo aliyoionyesha mwalimu huyo na kusema kuwa kwa upande wake atamchukulia hatua za kinidham kwani kitendo alichikifanya kinadidimiza jitihada za wananchi kuunga mkono serikali katika shughuli za kimaendeleo.

Tuesday, 9 January 2018

Wananchi Bunda stoo walidhishwa na huduma ya umeme ya REA



Wananchi wa kata Bunda stoo katika halmashauri ya mji wa Bunda mkoa wa Mara wameeleza namna wamenufaika na huduma ya umeme wa REA ikiwa ni pamoja na kijipatia maendeleo ya kiuchumi kutokana na huduma hiyo.
Hayo yamesemwana baadhi ya wananchi wa mashine ya maji na migungani wakati wakizungumza na mazingira hii leo wamesema huduma ya umeme wa REA umewafikia walengwa kwa gharama nafuu ya elfu ishirini na saba kuvuta umeme huo ambapo huduma hiyo imeanza mwaka jana .

Wameongeza kuwa wengi wao katika maeneo hayo wamenufaika na uhuduma hiyo na wanafaaidika kutokana na huduma hiyo kuwasaidia katika matumizi ya nyumbani ikiwemo mwanga na kuchaji simu pia wanajipatia uchumi kupitia huduma hiyo ikwa ni pamoja na miradi inayotegemea umeme huo kama kuchajisha simu kuwaingizia kipato.

Aidha wamemuomba diwani wa kata ya bunda stoo kutembelea wakazi wa maeneo hayo kuwasikiliza matatizo yao ikiwemo tatizo la maji ambapo limekuwa tatizo katika maeneo mbalimbali ya mji wabunda.

Maji safi na salama yamekuwa adimu kupatikana mtaa wa Migungani Halmashauri ya mji wa Bunda



Hali ya upatikanaji maji safi na salama katika mtaa wa Migungani kata ya Bunda stoo  halmashauri ya mji wa Bunda mkoa wa Mara hairidhishi kutokana na huduma hiyo kuwa hafifu katika eneo hilo.

Wakizungumza na mazingira fm kwa  nyakati tofauti  baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamesema  hali ya upatikanaji wa maji inazidi kuwa ngumu kutokana na ukame unaokabili maeneo.

Stivine Warioba mkazi wa migungani amedai kuwa mamlaka ya maji katika halmashauri ya mji BAWASA, wamekataa uuzaji wa maji katika mabomba ya watu binafsi kutokana kutojaza mikataba ya awali ya kuuza maji .

Naye mwenyekiti wa mtaa wa migungani bwana Elias Robati amekiri kuwepo tatizo la maji na tayari linafaniwa ufumbuzi ikiwemo kukusanya michango mbalimbali kutoka kwa wananchi kuweza kusambaza line kubwa ya mabomb.

Aidha wananchi hao wameiomba halmashauri ya mji huo kutatua tatizo hilo haraka kwani imekuwa ni kero kwani  wanawake na watoto ndiyo wenye kupata adha hiyo