Maji safi na salama yamekuwa adimu kupatikana mtaa wa Migungani Halmashauri ya mji wa Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Tuesday 9 January 2018

Maji safi na salama yamekuwa adimu kupatikana mtaa wa Migungani Halmashauri ya mji wa Bunda



Hali ya upatikanaji maji safi na salama katika mtaa wa Migungani kata ya Bunda stoo  halmashauri ya mji wa Bunda mkoa wa Mara hairidhishi kutokana na huduma hiyo kuwa hafifu katika eneo hilo.

Wakizungumza na mazingira fm kwa  nyakati tofauti  baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamesema  hali ya upatikanaji wa maji inazidi kuwa ngumu kutokana na ukame unaokabili maeneo.

Stivine Warioba mkazi wa migungani amedai kuwa mamlaka ya maji katika halmashauri ya mji BAWASA, wamekataa uuzaji wa maji katika mabomba ya watu binafsi kutokana kutojaza mikataba ya awali ya kuuza maji .

Naye mwenyekiti wa mtaa wa migungani bwana Elias Robati amekiri kuwepo tatizo la maji na tayari linafaniwa ufumbuzi ikiwemo kukusanya michango mbalimbali kutoka kwa wananchi kuweza kusambaza line kubwa ya mabomb.

Aidha wananchi hao wameiomba halmashauri ya mji huo kutatua tatizo hilo haraka kwani imekuwa ni kero kwani  wanawake na watoto ndiyo wenye kupata adha hiyo

No comments:

Post a Comment