Showing posts with label HABARI. Show all posts
Showing posts with label HABARI. Show all posts

Monday, 9 June 2025

Wazee 2 hadi 3 kati ya 10 hufanyiwa ukatili Bunda

 

Afisa ustawi wa jamii halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara Waryoba Juma

Baadhi ya wazee wameitaka serikali iwatambue wazee kwamba wapo, pia iwahudumie hasa katika sera ya matibabu bure kwa wazee maana wakati mwingine hukosa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya

Na Adelinus Banenwa

Imeelezwa kuwa wazee wawili (2)hadi watatu (3) kati ya wazee kumi (10) halmashauri ya mji wa Bunda hufanyiwa ukatili mbalimbali katika jamii na familia.

Hayo yamesemwa leo na afisa ustawi wa jamii halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara Waryoba Juma ambapo amesema takwimu hizo siyo nzuri lakini pia siyo mbaya ukilinganisha na maeneo mengine nchini.

Waryoba amesema ukatili wanaokutana nao wazee ni pamoja na kubaguliwa, kunyanyaswa, kutosikilizwa na wakati mwingine wazee wanapigwa  matukio ambayo matukio haya yanagawanyika katika makundi mawili ya unyanyasaji ambayo ni kimwili na kisaikolojia.

Waryoba ameyasema hayo katika kikao kilichowakutanisha wazee kutoka mitaa ya kata ya Sazira walipokuta na viongozi wa baraza la ushauri la wazee halmashauri ya mji wa Bunda.

Sauti ya Waryoba Juma

Kwa upande wao baadhi ya wazee wameitaka serikali iwatambue wazee na kwamba wapo pia iwahudumie hasa katika sera ya matibabu bure kwa wazee maana wakati mwingine hukosa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya pia watoto wao kushindwa kuwalea na badala yake huwarundikia wajukuu nyumbani bila utaratibu.

Baadhi ya wazee waliohudhulia kikao cha wazee Sazira
Sauti ya baadhi ya wazee

Naye Machael Kweka ambaye ni mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bunda na diwani wa kata ya Sazira  ameiomba serikali  kuleta mpango wa kulipa pensheni kwa wazee wa Tanzania bara kama inavyofanyika huko Zanzibar na lingine watoto wenye kazi kuhakikisha wanawakatia bima za matibabu wazee wao.

Sauti ya Michael Kweka

Sunday, 8 June 2025

Auawa na tembo akilinda shamba la Nyanya Bunda

 

Alikuwa analinda mazao yake yasiliwe na tembo na ndiyo kawaida yetu maana bila kulinda huwezi kuvuna chochote.

Na Adelinus Banenwa

Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la Kinyunyi Nyakile mkazi wa mtaa wa Ichamu kata ya Kunzugu Halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara amepteza maisha baada ya kushambuliwa na tembo wakati akilinda bustani yake ya nyanya.

Tukio hilo linatajwa kutokea usiku wa kuamkia Juni 8, 2025 ambapo inaelezwa kundi la tembo zaidi ya watano walifika karibu na mashamba ya wakulima hapo Kunzugu ndipo wakulima walianza kuwafukuza lakini tembo mmoja aligeuka na kuanza kuwakimbiza hadi alipomshika Kinyunyi na kumkanyaga vibaya hali iliyopelekea kupoteza maisha.

Mwenyekiti wa mtaa wa Ichamu James Magwayega Haruna ameiambia mazingira fm kuwa tukio hilo limewasikitisha kutokana na kupoteza nguvu kazi ya mtaa na imekuwa kawaida kwa wakazi wa mtaa wake ili wavune mazao yao ya shambani ni lazima kulinda.

Sauti ya Mwenyekiti wa mtaa wa Ichamu James Magwayega Haruna

Kwa upande wake Magambo Magambo ambaye ni baba mdogo wa marehemu Kinyunyi amesema kama familia wamepoteza mtu muhimu sana hasa ukizingatia alikuwa bado mdogo na alikuwa hajawa na familia Aidha ameiomba serikali kujenga uzio kuzuia wanyama hao ili kunusuru maisha ya wananchi na mazao.

Sauti ya Magambo Magambo ambaye ni baba mdogo wa marehemu

Naye diwani wa kata ya Kunzugu Mhe Pasaka Samson amesema taarifa za mwananchi wake alizipata usiku ambapo alichukua hatua ya kwenda hadi eneo la tukio kisha aliwasiliana na mamlaka mbalimbali ikiwemo watu wa Kikosi dhidi ya ujangiri KDU, Jeshi la polisi pamoja na ofisi ya mkuu wa wilaya.

Mhe Pasaka amesisitiza kuwa serikali ione umuhimu wa kuongeza gari la doria kwa kuwa lililopo halitoshi kuanzia Balili hadi Tungirima ambao ni ukanda wote wa hifadhi ya taifa ya Serengeti.

Sauti ya diwani wa kata ya Kunzugu Mhe Pasaka Samson

Friday, 6 June 2025

Wafugaji kufanya kongamano kubwa June, 15 na 16

 

Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Ndugu Mrida Mshota

Watu zaidi ya laki moja wakitalajiwa kuudhulia katika kongamano hilo

Na Thomas Masalu

Chama cha Wafugaji Tanzania kimetangaza kufanyika kwa kongamano maalum la siku mbili litakalofanyika tarehe 15 na 16 Juni mwaka huu, katika viwanja vya nane nane , Nyakabindi mkoani Simiyu huku watu zaidi ya laki moja wakitalajiwa kuudhulia katika kongamano hilo linalolenga uzinduzi wa chanjo ya mifugo na utambuzi pamoja na kujadili changamoto na fursa zilizopo katika sekta ya ufugaji nchini.

Akizungumza na Redio Mazingira FM, leo tarehe 6/6/2025 kupitia kipindi cha Duru za Habari, Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Ndugu Mrida Mshota, amesema kuwa maandalizi ya kongamano hilo yanaendelea vizuri.

Aidha mwenyekiti huyo wa chama cha wafugaji Tanzania Mrida Mshota ameeleza kuwa Mgeni Rasmi katika Kongamano hilo maaalum la siku mbili, anatarajiwa kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Daktari Samia Suluhu Hassan,

Sauti ya Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Ndugu Mrida Mshota

Huku akiongeza kuwa kongamano hilo linalotarajiwa kuwahusisha wafugaji kutoka mikoa mbalimbali nchini, huku likitarajia kutoa afua ya masuala ya sera za ufugaji, teknolojia mpya, masoko ya bidhaa za mifugo, pamoja na umuhimu wa uhifadhi wa mazingira katika shughuli za ufugaji.

kwa Kuwa ni mara ya ya kwanza kwa Tanzania kuwa na kongamano la kitaifa la utoaji chanjo na utambuzi kwa mifugo jambo ambalo limefanyika katika uongozi wa awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Sauti ya Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Ndugu Mrida Mshota

Wednesday, 4 June 2025

Vikundi vya ulinzi shirikishi hupunguza uhalifu kwenye jamii

 

Mkaguzi wa polisi Jonas Kaijage ambaye ni mratibu wa polisi jamii wilayani Bunda

Bunda kuna jumla ya vikundi 31 vya ulinzi shirikishi ambavyo vipo hai na katika maeneo hayo matukio ya uharifu yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Na Adelinus Banenwa

Imeelezwa kuwa sehemu zenye vikundi vya ulinzi shirikishi yaani polisi jamii wilayani Bunda matukio ya kiharifu yamepungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na maeneo ambayo hakuna kabisa vikundi hivyo.

Hayo yamesemwa na mkaguzi wa polisi Jonas Kaijage ambaye ni mratibu wa polisi jamii wilayani Bunda kupitia kipindi cha Asubuhi leo kinachorushwa Radio Mazingira fm ambapo amesema kwa wilaya ya Bunda kuna jumla ya vikundi 31 vya ulinzi shirikishi ambavyo vipo hai na katika maeneo hayo matukio ya uharifu yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Kaijage ameongeza kuwa sheria ya kuwepo kwa ulinzi shirikishi una lengo la kuishirikisha jamii katika masuala ya ulinzi na usalama katika maeneo yao ndiyo maana kama jeshi la polisi wanahusika kutoa elimu na maelekezo kwa vikundi vinavyoanzishwa.

Kaijage ametoa wito kwa jamii kuhakikisha kupitia kwa wenyeviti wa mitaa, vijiji na vitongoji wanaanzisha vikundi hivyo ili kuweka usalama kwenye maeneo yao kwa kuwa sasa jeshi la polisi limesogeza karibu kabisa huduma na vikundi hivyo ikiwa nipamoja na kila kata kuwepo kwa polisi kata ambaye anasaidia kutoa elimu kwa vikundi hivyo.

Sauti ya Jonas Kaijage ambaye ni mratibu wa polisi jamii wilayani Bunda

Kwa upande mwingine Insp Kaijage amewataka wafanyabiashara wanaotoa huduma za kifedha kwa maana ya huduma pesa kuwa waangalifu kutokana na changamoto za wizi na utapeli ambao unaonekana kushamili kwa siku za hivi karibuni.

Sauti ya Jonas Kaijage ambaye ni mratibu wa polisi jamii wilayani Bunda

Thursday, 29 May 2025

Wananchi wahimizwa kutunza na kuwahifadhi kobe

 

Lusato Masinde Afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ya ziwa ,picha na Catherine Msafiri

Kobe ni wanyama kama walivyo wanyamapori wengine na wanalindwa kisheria tuwatunze.

Na Catherine Msafiri,

Jamii imetakiwa kuendelea kuwatunza na kuwalinda kobe kwaajiri ya manufaa ya vizazi vijavyo kwani ujangili dhidi yao unahatarisha uwepo wa mnyama kobe kwa miaka ijayo.

Hayo yameelezwa na afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ya ziwa ndugu,Lusato Masinde alipofanya mahojiano na radio Mazingira fm kwenye kipindi cha uhifadhi na utalii.

Afisa wanyamapori TAWA kanda ya ziwa Lusato Masinde

Aidha Masinde ameeleza kuwa binadamu ndie kiumbe hatari zaidi kwa mnyama kobe kutokana na shughuli zao hasa pindi wanapochoma misitu
Pia amebainisha kuwa mnyama kobe anafaida mbalimbali kiuchumi, kiikolojia na kijamii

Sauti ya Afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ziwa Lusato Masinde

Hata hivyo ameeleza sifa za mnyama kobe huku akibainisha kuwa kisheria watu wanaweza kuanzisha mashamba ya kufuga kobe isipokuwa tu kwa kuzingatia sheria na taratibu.

Sauti ya Afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ziwa Lusato Masinde

Thursday, 8 May 2025

Upatikanaji wa samaki wengi waathiri biashara ya nyama Bunda

 

Wateja wamepungua kwa kasi katika siku za hivi karibuni kutokana na watu wengi kuelekeza nguvu zao katika kununua samaki

Na Thomas Masalu

Imeelezwa kuwa katika mji wa Bunda, upatikanaji mkubwa wa samaki kwa sasa umeanza kuathiri kwa kiasi kikubwa biashara ya nyama ya ng’ombe, hali inayowatia hofu baadhi ya wafanyabiashara wa nyama hiyo.

Wafanyabiashara hao wamesema kuwa wateja wamepungua kwa kasi katika siku za hivi karibuni kutokana na watu wengi kuelekeza nguvu zao katika kununua samaki ambao wanapatikana kwa wingi sokoni.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti leo Mei 7, 2025, na redio Mazingira FM katika eneo la genge la jioni, wafanyabiashara hao wameeleza kuwa tofauti ya bei kati ya samaki na nyama ya ng’ombe imechangia kushuka kwa mzunguko wa biashara yao.

Wafanyabiashara hao wamesema kuwa licha ya changamoto hiyo, bado wana matumaini kuwa hali itabadilika pindi upatikanaji wa samaki utakapopungua.

Sauti ya Wafanyabiashara

Tuesday, 6 May 2025

Waliolipwa Nyatwali watakiwa kuondoka

 

Mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi

Serikali tayari imetoa bilioni 53 kwa ajili ya ulipaji wa fidia kwa wakazi hao ili kuachia maeneo hayo yawe sehemu ya hifadhi ya taifa ya Serengeti.

Na Adelinus Banenwa

Wananchi wa Nyatwali ambao tayari wamelipwa stahiki zao kwa utaratibu wa kisheria watakiwa kuondoka.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya urithi wa dunia na afrika yaliyofanyika wilayani Serengeti mkoani Mara leo tarehe 5 May 2025.

Kanal Mtambi amesema serikali tayari imetoa bilioni 53 kwa ajili ya ulipaji wa fidia kwa wakazi hao ili kuachia maeneo hayo yawe sehemu ya hifadhi ya taifa ya Serengeti.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria maadhimisho ya siku ya urithi duniani

Kanal Mtambi amesema eneo la Nyatwali tangu enzi za ukoloni lilionekana si sehemu salama kwa makazi ya binadamu na wakati huo lilitambulika kama guba ya speek na utaratibu wa wananchi waliokuwa eneo hilo kuhamishwa ulianza muda mrefu lakini serikali ya awamu ya sita imefanikisha jambo hilo.

Aidha mkuu wa mkoa wa Mara amesema kiasi cha malipo kilichosalia kinaendelea kulipwa kwa utaratibu uliowekwa

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi

Thursday, 1 May 2025

Aliyemchoma mtoto wake mkono ahukumiwa, Bunda

 

Katika utetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama imuachie huru kutokana na yeye kuwa ni mjane na ana watoto watano wanamtegemea.

Na Adelinus Banenwa

Mahakama ya wilaya ya Bunda imemuhukumu kifungo cha masharti (condition discharge) cha kutokutenda kosa lolote ndani ya miezi sita Neema Msimu John(28), Mkazi wa mtaa wa Mapinduzi kwa kosa la ukatali dhidi ya mtoto wake mwenye umri wa miaka minne kwa kumchoma moto kwenye mkono wake wa kushoto kwa kosa la kujisaidia hovyo.

Hukumu hiyoimetolewa na Hakimu mkazi Mwandamizi wa mahakama ya wilaya ya Bunda, Betron Sokanya, baada ya mshitakiwa kukiri kutenda kosa hilo ambalo ni kinyume na kifungu Cha 169A(1)  na (2) cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2022.

Katika utetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama imuachie huru kutokana na yeye kuwa ni mjane na ana watoto watano wanamtegemea huku mmoja wapo akiwa ananyonya.

Neema Msimu John

Awali kabla ya hukumu kutolewa, mwendesha Mashtaka wa Jamuhuri Aristariko Msongelo ameiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwefundisho kwa jamii kuacha tabia ya ukatili dhidi ya watoto.

‘‘Naomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwe fundisho kwa jamii kuacha tabia ya ukatili dhidi ya watoto’’. Aristariko Msongelo mwendesha mashitaka wa Jamhuri Wilaya ya Bunda.

Aidha Afisa ustawi wa jamii Wilaya ya Bunda Florence Debogo awewaasa wazazi kutotumia adhabu kali kwa watoto na badala yake watumie adhabu mbadala kama kumnyima mtoto kuangalia television na kuto kwenda kucheza ili kupunguza wimbi la ukatili kwa watoto.

Saturday, 26 April 2025

Kiwango cha malaria mkoa wa Mara asilimia 15

 

Wito umetolewa kwa wananchi kuzingatia usafi wa mazingira na matumizi sahihi ya vyandarua ili kuepuka maambukizi ya malaria

Hayo yamesemwa leo na Dr Henry Lukamisa ambaye ni mratibu wa Malaria mkoa wa Mara wakati akizungumza kupitia Radio Mazingira fm ndani ya kipindi cha Asubuhi leo

Amesema hadi sasa kwa mkoa wa Mara kiwango cha ugonjwa wa malaria ni asilimia 15.

Dr Henry Lukamisa ambaye ni mratibu wa Malaria mkoa wa Mara

Dr Henry amesema ugonjwa wa malaria umeua watoto takribani 62 kwa mkoa wa Mara kwa mwaka 2024 kwa vifo vilivyorekodiwa hivyo ni vema wananchi wakachukua tahadhari

Dr Henry Lukamisa

Naye Mohamed Mlanza ambaye ni mratibu wa malaria halmashauri ya mji wa Bunda ambapo amesema kwa halmashauri hiyo wanajitahidi kutekeleza afua mbalimbali za kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa malaria ikiwa ni pamoja na kugawa vyandarua kwa mama wajawazito na kwa akina mama wenye watoto wachanga.

Mohamed Mlanza ambaye ni mratibu wa malaria

Aidha Mlanza ameongeza kuwa mbali na kutoa vyandarua pia idara hiyo inatoa elimu kwa jamii juu ya namna unavyoenezwa na kusambaa pamoja na madhara ugonjwa huo.

Mohamed Mlanza

Ikumbukwe kuwa kila tarehe 25 April kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya malaria ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ni ” Malaria inatokomezwa na sisi, wekeza chukua hatua, ziro malaria inaanza na mimi”

Wednesday, 23 April 2025

Mwalimu jela miaka 30 kwa ubakaji, ulawiti

 

Mbali na kifungo cha miaka 30 pia mahakama imeamuru kulipa fidia ya shilingi milioni 2 kwa muhanga kwa mujibu wa sheria ya uendeshaji wa makosa ya jinai 348 (1) sura ya 20 marejeo ya mwaka 2022.

Na Adelinus Banenwa

Mahakama ya wilaya ya Bunda imemuhukumu kifungo cha miaka 30 jela na fidia ya shilingi milioni 2 Vicent Joseph Nkunguu (39) aliyekuwa mwalimu mkuu wa shule msingi masaunga wilayani Bunda kwa kosa la ubakaji na ulawiti wa mwanafunzi (16) wa darasa la sita ambaye jina lake limehifadhiwa.

Hukumu hiyo ya kesi ya jinai namba 7623 ya mwaka 2024 imetolewa leo tarehe 23 April 2025 na hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama ya wilaya ya Bunda mhe Betron Sokanya

Akisoma hukumu hiyo Mhe Sokanya amesema mahakama imejiridhisha bila kuacha shaka kuwa mtuhumiwa Vicent Joseph Nkungu alitenda kosa hilo baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili ambapo upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi watano (5) na kielelezo kimoja huku upande wa utetezi ukiwasilisha mashahidi wawili (2) bila kielelezo chochote.

Mhe Sokanya amesema katika kosa la kwanza la ubakaji mahakama imemtia hatiani kutokana na mshitakiwa huyo kutenda kosa angali akijua ni kinyume na kifungu cha 130 (1) (2)( e) na kifungu cha 131 (1) cha sheria ya kanuni ya adhabu sura 16 marejeo ya mwaka 2022

Aidha katika kosa la pili la kulawiti Mhe Sokanya amesema mahakama imemkuta mshitakiwa na hatia kinyume na kifungu cha cha 154 (1) (a) cha kanuni ya adhabu sura 16 marejeo ya mwaka 2022.

Mbali na kifungo cha miaka 30 pia mahakama imeamuru mshitakiwa Vicent kulipa fidia ya shilingi milioni 2 kwa muhanga kwa mujibu wa sheria ya uendeshaji wa makosa ya jinai 348 (1) sura ya 20 marejeo ya mwaka 2022.

Awali Mwendesha mashtaka wa serikali Isiaka Ibrahim Mohamed alisema matukio hayo yalitendeka tarehe 9 March 2024 nyumbani kwa mshitakiwa huku mwendesha mashtaka akiiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili liwe fundisho kwake na kwa wengine wenye tabia kama zake

Katika utetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama impunguzie adhabu kwa sababu ni mara yake ya kwanza kukutwa na hatia pia ana mke na watoto wanaomtegemea.

Mhe hakimu Sokanya amesema rufaa ipo wazi kwa hukumu hiyo.

Tuesday, 22 April 2025

Radio jamii zanolewa kumulika nafasi ya wanawake uchaguzi mkuu 2025

 

Picha ya pamoja washiriki wa mafunzo kwa radio jamii Tanzania yaliyotolewa na TAMWA kwa kushirikiana na TADIO jijiji Dodoma

Licha ya sensa ya watu na makazi ya 2022 kuonesha idadi ya wanawake ni wengi kuliko wanaume, katika nafasi za uongozi kwa ngazi za udiwani na ubunge bado kuna idadi ndogo zaidi ya uwakilishi.

By Edward Lucas

Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania TAMWA kwa kushirikiana na TADIO wameendesha mafunzo kwa radio za kijamii Tanzania Bara kuandaa habari na vipindi vitakavyowawezesha wanawake kushiriki kikamilifu hasa kwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu wa 2025.

Akizungumzia mafunzo hayo, Meneja Mipango na Mikakati TAMWA, Sylivia Daulinge amesema mafunzo hayo yanayodhaminiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Vyombo vya Habari Finland VIKES yamelenga elimu ya namna bora ya kuandaa vipindi vya usawa na ujumuishi wa masuala ya kijinsia kwa kuhakikisha wanawake hasa vijana na makundi maalumu yanapewa kipaumbele kuelekea uchaguzi mkuu.

Sylivia Daulinge, Meneja Mipango na Mikakati TAMWA
Sylivia Daulinge, Meneja Mipango na Mikakati TAMWA

Kwa upande wake Mkufunzi wa mafunzo hayo kutoka Radio Tadio, Hilali Alexander Ruhundwa amesema kwa kushirikiana na TAMWA wameona wanajukumu la kufanya katika jamii kwa kuwashirikisha waandishi wa habari ili kufikisha elimu kwa jamii kuwafanya wanawake washiriki kikamilifu katika uchaguzi ujao

Hilali Alexander Ruhundwa, Mkufunzi wa mafunzo kutoka Radio Tadio akieleza kuhusu malengo ya mafunzo kwa radio za jamii kuelekea uchaguzi wa 2025
Sauti ya Hilali Alexander Ruhundwa

Kwa takwimu za uchaguzi mkuu uliopita wa mwaka 2020, madiwani wanawake waliochaguliwa kwenye kata ni 260 kati ya 3,953 ambao ni sawa na asilimia 6.58 na kwa upande wa ubunge kati ya majimbo 264 wabunge wanawake waliochaguliwa kwenye majimbo ni 26 tu sawa na asilimia 9.85