Wito umetolewa kwa wananchi kuzingatia usafi wa mazingira na matumizi sahihi ya vyandarua ili kuepuka maambukizi ya malaria
Hayo yamesemwa leo na Dr Henry Lukamisa ambaye ni mratibu wa Malaria mkoa wa Mara wakati akizungumza kupitia Radio Mazingira fm ndani ya kipindi cha Asubuhi leo
Amesema hadi sasa kwa mkoa wa Mara kiwango cha ugonjwa wa malaria ni asilimia 15.

Dr Henry amesema ugonjwa wa malaria umeua watoto takribani 62 kwa mkoa wa Mara kwa mwaka 2024 kwa vifo vilivyorekodiwa hivyo ni vema wananchi wakachukua tahadhari
Naye Mohamed Mlanza ambaye ni mratibu wa malaria halmashauri ya mji wa Bunda ambapo amesema kwa halmashauri hiyo wanajitahidi kutekeleza afua mbalimbali za kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa malaria ikiwa ni pamoja na kugawa vyandarua kwa mama wajawazito na kwa akina mama wenye watoto wachanga.

Aidha Mlanza ameongeza kuwa mbali na kutoa vyandarua pia idara hiyo inatoa elimu kwa jamii juu ya namna unavyoenezwa na kusambaa pamoja na madhara ugonjwa huo.
Ikumbukwe kuwa kila tarehe 25 April kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya malaria ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ni ” Malaria inatokomezwa na sisi, wekeza chukua hatua, ziro malaria inaanza na mimi”
No comments:
Post a Comment