Mwalimu jela miaka 30 kwa ubakaji, ulawiti - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Wednesday, 23 April 2025

Mwalimu jela miaka 30 kwa ubakaji, ulawiti

 

Mbali na kifungo cha miaka 30 pia mahakama imeamuru kulipa fidia ya shilingi milioni 2 kwa muhanga kwa mujibu wa sheria ya uendeshaji wa makosa ya jinai 348 (1) sura ya 20 marejeo ya mwaka 2022.

Na Adelinus Banenwa

Mahakama ya wilaya ya Bunda imemuhukumu kifungo cha miaka 30 jela na fidia ya shilingi milioni 2 Vicent Joseph Nkunguu (39) aliyekuwa mwalimu mkuu wa shule msingi masaunga wilayani Bunda kwa kosa la ubakaji na ulawiti wa mwanafunzi (16) wa darasa la sita ambaye jina lake limehifadhiwa.

Hukumu hiyo ya kesi ya jinai namba 7623 ya mwaka 2024 imetolewa leo tarehe 23 April 2025 na hakimu mkazi mwandamizi wa mahakama ya wilaya ya Bunda mhe Betron Sokanya

Akisoma hukumu hiyo Mhe Sokanya amesema mahakama imejiridhisha bila kuacha shaka kuwa mtuhumiwa Vicent Joseph Nkungu alitenda kosa hilo baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili ambapo upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi watano (5) na kielelezo kimoja huku upande wa utetezi ukiwasilisha mashahidi wawili (2) bila kielelezo chochote.

Mhe Sokanya amesema katika kosa la kwanza la ubakaji mahakama imemtia hatiani kutokana na mshitakiwa huyo kutenda kosa angali akijua ni kinyume na kifungu cha 130 (1) (2)( e) na kifungu cha 131 (1) cha sheria ya kanuni ya adhabu sura 16 marejeo ya mwaka 2022

Aidha katika kosa la pili la kulawiti Mhe Sokanya amesema mahakama imemkuta mshitakiwa na hatia kinyume na kifungu cha cha 154 (1) (a) cha kanuni ya adhabu sura 16 marejeo ya mwaka 2022.

Mbali na kifungo cha miaka 30 pia mahakama imeamuru mshitakiwa Vicent kulipa fidia ya shilingi milioni 2 kwa muhanga kwa mujibu wa sheria ya uendeshaji wa makosa ya jinai 348 (1) sura ya 20 marejeo ya mwaka 2022.

Awali Mwendesha mashtaka wa serikali Isiaka Ibrahim Mohamed alisema matukio hayo yalitendeka tarehe 9 March 2024 nyumbani kwa mshitakiwa huku mwendesha mashtaka akiiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili liwe fundisho kwake na kwa wengine wenye tabia kama zake

Katika utetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama impunguzie adhabu kwa sababu ni mara yake ya kwanza kukutwa na hatia pia ana mke na watoto wanaomtegemea.

Mhe hakimu Sokanya amesema rufaa ipo wazi kwa hukumu hiyo.

No comments:

Post a Comment