Saturday, 24 March 2018
Friday, 23 March 2018
Tafuteni suluhu ya pamoja ili kuzuia wanyama pori waharibifu mashambani-Bunda Mara
Wakazi wa vijiji vinavyopakana
na hifadhi ya taifa ya Serengeti
wamehamasishwa kutafuta suluhu ya pamoja ili kuzuia wanyama pori waharibifu
ambao wamekuwa changamoto katika vijiji vyao.
Akizungumza na
wananchi wa kijiji cha Tingirima kilichopo kata ya Mugeta
wilayani Bunda mwakilishi kutoka kampuni
ya wawekezaji ya Grumet Fund David Mwakipesile
ambao pia ni waratibu wa elimu hiyo
amesema kuwa kama kampuni wameamua kutoa elimu hiyo kwa vijiji vyote vya
wilaya ya Bunda hasa vijiji vya Mugeta, kyandege, sarakwa,mariwanda,kihumbu,hunyari,
nyamatoke,bukhore, kunzugu na kumaliza na kijiji cha balili kwa kusudi la
kuweka mikakati ya pamoja ya kuzuia wanyama pori waharibifu.
Mwakipesile amewaambia
wanaTingirima kuwa wao kama kampuni
baada ya kuona tatizo la wanyama
waharibifu kama tatizo la kitaifa wameamua kuanzisha kikosi maalum
kinachosaidia kufukuza wanyama hao na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kikosi hicho .
Naye afisa Wanyama pori wilaya ya Bunda Marwa Kitende
amesema kuwa lengo la serikali siyo
kulipa fidia ama kifuta machozi kwa
wananchi bali lengo lao ni kuhakikisha
wanazuia wanyama hao kabla hawajafanya uharibifu.
Wednesday, 21 March 2018
Jeshi la polisi la kanusha kusababisha ajali ya mwanafunzi wa darasa la pili -Bunda Mara
Wanafunzi katika shule
ya msingi Balili B halmashauri ya mji wa Bunda Mkoani Mara wameandamana mapema
leo asubuhi hadi zilipo ofisi ya mkurugenzi wa mji baada ya mwenzao
kugongwa kwa gari na kupelekea kifo
chake katika kivuko cha watembea kwa miguu kilichopo karibu na shule hiyo.
Tukio hilo la kugongwa kwa gari hadi kufa limempata Mwanafunzi wa darasa la sita aitwae Julius Nyerere mwenye umri wa miaka 12 na mwili wake umehifadhiwa katika hospitali teuli ya wilaya ya Bunda DDH.
Mashuhuda wa Tukio hilo wamesema wameshuhudia mwanafunzi huyo akigongwa kwa gari lenye rangi ya Dark blue ambalo wao wamelihusisha na gari la askari mmoja wa jeshi la polisi.
Tukio hilo la kugongwa kwa gari hadi kufa limempata Mwanafunzi wa darasa la sita aitwae Julius Nyerere mwenye umri wa miaka 12 na mwili wake umehifadhiwa katika hospitali teuli ya wilaya ya Bunda DDH.
Mashuhuda wa Tukio hilo wamesema wameshuhudia mwanafunzi huyo akigongwa kwa gari lenye rangi ya Dark blue ambalo wao wamelihusisha na gari la askari mmoja wa jeshi la polisi.
Kufuatia tukio hilo
mwalimu flora isack anaefundisha katika shule hiyo amewalalamikia baadhi ya
askari wa jeshi la polisi kumpiga na kumdhalilisha kwa kumvua nguo kwa kile
alichoeleza kwamba alihusika kuhamasisha wanafunzi kufunga barabara na kuponda kwa
mawe baadhi ya magari ya abiria yaliyokuwa yakipita kuelekea mwanza na musoma.
Kwa upende wa jeshi la polisi wilaya ya Bunda kupitia kwa OCD Jeremia Shila amekiri kutokea kwa tukio
hilo la mwanafunzi kugongwa kwa gari hadi kufa ambapo amesema kuwa jeshi la
polisi linaendelea na ufuatiliaji wa gari lililohusika na ajili hiyo.
Kwa upande wa madai ya
askari wa polisi kuhusishwa na ajali hiyo pamoja na kumshambulia mwali huyo
kamanda shila amepinga taarifa hizo na kueleza kuwa tukio hilo limesababishwa
na kijana mmoja ambae baadae gari lake lililohusika na ajali limeonekana musoma
na wanaendelea kulifuatilia ambapo ameaidi kutoa taarifa kwa umma pindi
watakapokamilisha utaratibu wa kumkamata mhusika.
Aidha kuhusu mwalimu
flora kushambuliwa amesame hakushambuliwa badala yake alikuwa akiondolewa
barabarani kupisha watumiaji wengine wa barabara kuendelea na shughuli zao.
Monday, 19 March 2018
Wake za Marehemu Wafichua Mazito, Kifo cha Mmiliki wa Super Sami
Mapya
yameibuka kufuatia kifo cha mfanyabiashara mabye ni tajiri wa mabasi ya kampuni
ya Super Sami, Samson Josiah almaarufu Super Sami, mkazi wa Magu Mwanza, baada
ya wake zake kufunguka na kueleza ya moyoni kuhusu tukio hilo la kusikitisha
huku mkewe mdogo akimfichua anayemhisi kuwa muuaji.
Mfanyabiashara
huyo alipotea katika mazingira ya kutatanisha kwa siku kadhaa kabla ya mwili
wake kuonekana katika mto Ndabaka, wilayani Bunda Mkoani Mara ukiwa umefungwa
kwenye kiroba na kuharibika vibaya.
Kwa nyakati
tofauti wake wa marehemu walizungumza na Ijumaa Wikienda na kutoa maoni yao,
huku wakieleza mambo wanayoamini kuwa yanaweza kuchangia kifo cha mume wao.
Mange kimambi aibukia tarime.
Mbunge wa Serengeti,mkoani Mara
Marwa Ryoba Chacha (CHADEMA) ameonyesha kutofurahishwa na kitendo cha polisi
kutaka kuzuia mkutano wa Mbunge wa Tarime Vijijini CHADEMA, Mhe. John Heche kwa
kile kinachodaiwa kuhofia maandamano yanayoratibiwa na Mange Kimambi.
Marwa Ryoba amesema kuwa polisi
wamekuwa na upendeleo kwa kuwa wanaona watu wa CCM wakiendelea kufanya
maandamano na mikutano ya kisiasa ili hali watu wa upinzani wakizuiliwa.
"Haki huinua taifa; bali dhambi
ni aibu ya watu wote. Nimepata taarifa kwamba Mbunge wa Tarime vijijini Mh.
John Heche alizuiliwa asifanye mkutano Sirari eti kisa kuna maandamano ya Mange
Kimambi, kwanza maandamano sio dhambi yapo kwa mujibu wa katiba yetu"
,alisema Mbunge Marwa Ryoba
Kwa mujibu wa Mbunge wa Tarime Vijijini
kwa tiketi ya CHADEMA, John Heche amethibitisha hilo kuwa ni kweli kulikuwa na
jaribio la kutaka kuzuiwa kufanya mkutano wake na wananchi wa Sirari kwa hofu
ya maandamano ya tarehe 26 mwezi wa nne.
"Ni kweli polisi walitaka
kutuzuia kufanya mkutano ila pamoja na polisi Sirari kufanya jaribio la kutaka
kuzuia mkutano wangu na wananchi, kwa kisingizio cha hofu ya maandamano ya
tarehe 26. Mkutano wangu ulifanyika na umemalizika salama, Asanteni sana wananchi
wa Sirari kwa kujitokeza kwenye mkutano wetu" alisema John Heche.
Subscribe to:
Posts (Atom)