Wake za Marehemu Wafichua Mazito, Kifo cha Mmiliki wa Super Sami - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Monday 19 March 2018

Wake za Marehemu Wafichua Mazito, Kifo cha Mmiliki wa Super Sami

                      

Mapya yameibuka kufuatia kifo cha mfanyabiashara mabye ni tajiri wa mabasi ya kampuni ya Super Sami, Samson Josiah almaarufu Super Sami, mkazi wa Magu Mwanza, baada ya wake zake kufunguka na kueleza ya moyoni kuhusu tukio hilo la kusikitisha huku mkewe mdogo akimfichua anayemhisi kuwa muuaji.

Mfanyabiashara huyo alipotea katika mazingira ya kutatanisha kwa siku kadhaa kabla ya mwili wake kuonekana katika mto Ndabaka, wilayani Bunda Mkoani Mara ukiwa umefungwa kwenye kiroba na kuharibika vibaya. 

Kwa nyakati tofauti wake wa marehemu walizungumza na Ijumaa Wikienda na kutoa maoni yao, huku wakieleza mambo wanayoamini kuwa yanaweza kuchangia kifo cha mume wao.

No comments:

Post a Comment