NABII MTOTO TAJIRI: Anayegawa Pesa, Anaponyesha Ukimwi..! - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Tuesday 6 March 2018

NABII MTOTO TAJIRI: Anayegawa Pesa, Anaponyesha Ukimwi..!




KILA kukicha wanatokea manabii wanaokuja na staili mbalimbali za mahubiri na miujiza ya kila aina, wakati Nabii Tito ambaye alikuwa akihubiri mitaani kwamba kuzini na kulewa siyo dhambi, akisota Hospitali ya Mirembe mkoni Dodoma, baada ya kuonekana kwamba ana matatizo ya akili, mwingine aliyetambulika kwa jina la Daniel Daniel Shilla (22), ameibuka na kutikisa Jiji la Dar. Nabii huyo mtoto ambaye ni gumzo kwenye mitandao ya kijamii kutokana na kugawa pesa kwa waumini wanaosali kanisani kwake, anaongoza kanisa linalojulikana kwa jina la Bethel International Ministry Of Tanzania, lililopo kwenye Viwanja vya Sabasaba na Kigamboni kwa jijini Dar na matawi mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Zanzibar, Kigoma, Morogoro na mengineyo. 

Baada ya kuwepo kwa tuhuma nzito za kuwa na utajiri mkubwa usiokuwa na vielelezo, kuusishwa na Freemasons na masuala ya utapeli kwa wanaohitaji huduma zake za maombezi, Ijumaa Wikienda liliamua kumsaka Nabii Shilla na kukuletea stori kamili.

No comments:

Post a Comment