Tafuteni suluhu ya pamoja ili kuzuia wanyama pori waharibifu mashambani-Bunda Mara - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Friday 23 March 2018

Tafuteni suluhu ya pamoja ili kuzuia wanyama pori waharibifu mashambani-Bunda Mara



Wakazi  wa  vijiji   vinavyopakana  na hifadhi ya taifa ya Serengeti  wamehamasishwa kutafuta suluhu ya pamoja ili kuzuia wanyama pori waharibifu ambao wamekuwa changamoto katika vijiji vyao.

Akizungumza  na  wananchi  wa kijiji  cha Tingirima kilichopo kata ya Mugeta wilayani  Bunda mwakilishi kutoka kampuni ya wawekezaji  ya Grumet Fund David Mwakipesile  ambao  pia ni waratibu  wa elimu hiyo  amesema kuwa kama kampuni wameamua kutoa elimu hiyo kwa vijiji vyote vya wilaya ya Bunda hasa vijiji vya Mugeta, kyandege, sarakwa,mariwanda,kihumbu,hunyari, nyamatoke,bukhore, kunzugu na kumaliza na kijiji cha balili kwa kusudi la kuweka mikakati ya pamoja ya kuzuia wanyama pori waharibifu.

Mwakipesile  amewaambia  wanaTingirima kuwa wao kama kampuni baada ya kuona tatizo la wanyama  waharibifu kama tatizo la kitaifa wameamua kuanzisha kikosi maalum kinachosaidia kufukuza wanyama hao na kuwataka wananchi  kutoa ushirikiano kwa kikosi hicho .

Naye afisa Wanyama pori wilaya ya Bunda Marwa Kitende  amesema kuwa lengo la serikali siyo kulipa fidia ama kifuta machozi  kwa wananchi  bali lengo lao ni kuhakikisha wanazuia wanyama hao kabla hawajafanya uharibifu.

No comments:

Post a Comment