Watu zaidi ya laki moja wakitalajiwa kuudhulia katika kongamano hilo
Na Thomas Masalu
Chama cha Wafugaji Tanzania kimetangaza kufanyika kwa kongamano maalum la siku mbili litakalofanyika tarehe 15 na 16 Juni mwaka huu, katika viwanja vya nane nane , Nyakabindi mkoani Simiyu huku watu zaidi ya laki moja wakitalajiwa kuudhulia katika kongamano hilo linalolenga uzinduzi wa chanjo ya mifugo na utambuzi pamoja na kujadili changamoto na fursa zilizopo katika sekta ya ufugaji nchini.
Akizungumza na Redio Mazingira FM, leo tarehe 6/6/2025 kupitia kipindi cha Duru za Habari, Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Ndugu Mrida Mshota, amesema kuwa maandalizi ya kongamano hilo yanaendelea vizuri.
Aidha mwenyekiti huyo wa chama cha wafugaji Tanzania Mrida Mshota ameeleza kuwa Mgeni Rasmi katika Kongamano hilo maaalum la siku mbili, anatarajiwa kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Daktari Samia Suluhu Hassan,
Huku akiongeza kuwa kongamano hilo linalotarajiwa kuwahusisha wafugaji kutoka mikoa mbalimbali nchini, huku likitarajia kutoa afua ya masuala ya sera za ufugaji, teknolojia mpya, masoko ya bidhaa za mifugo, pamoja na umuhimu wa uhifadhi wa mazingira katika shughuli za ufugaji.
kwa Kuwa ni mara ya ya kwanza kwa Tanzania kuwa na kongamano la kitaifa la utoaji chanjo na utambuzi kwa mifugo jambo ambalo limefanyika katika uongozi wa awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
No comments:
Post a Comment