Serikali tayari imetoa bilioni 53 kwa ajili ya ulipaji wa fidia kwa wakazi hao ili kuachia maeneo hayo yawe sehemu ya hifadhi ya taifa ya Serengeti.
Na Adelinus Banenwa
Wananchi wa Nyatwali ambao tayari wamelipwa stahiki zao kwa utaratibu wa kisheria watakiwa kuondoka.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya urithi wa dunia na afrika yaliyofanyika wilayani Serengeti mkoani Mara leo tarehe 5 May 2025.
Kanal Mtambi amesema serikali tayari imetoa bilioni 53 kwa ajili ya ulipaji wa fidia kwa wakazi hao ili kuachia maeneo hayo yawe sehemu ya hifadhi ya taifa ya Serengeti.

Kanal Mtambi amesema eneo la Nyatwali tangu enzi za ukoloni lilionekana si sehemu salama kwa makazi ya binadamu na wakati huo lilitambulika kama guba ya speek na utaratibu wa wananchi waliokuwa eneo hilo kuhamishwa ulianza muda mrefu lakini serikali ya awamu ya sita imefanikisha jambo hilo.
Aidha mkuu wa mkoa wa Mara amesema kiasi cha malipo kilichosalia kinaendelea kulipwa kwa utaratibu uliowekwa
No comments:
Post a Comment