Thursday, 8 May 2025

Aswege: Halmashauri toeni elimu ya mikopo kwa wanawake wajasiriamali

 

Mkuu wa wilaya ya Bunda  Mhe Aswege Enock Kaminyoge

Tangu kuanzishwa kwa jukwaa hili mwaka 2005 limesaidia wanawake wengi katika kuhakikisha wanazifikia ndoto zao

Na Adelinus Banenwa

Mkuu wa wilaya ya Bunda  Mhe Aswege Enock Kaminyoge amezielekeza halmashauri za wilaya ya Bunda kuandaa program maalumu kwa ajili ya kutoa elimu ya mikopo kwa akina mama wajasiriamali ambao wanajiunga katika vikundi ili kupunguza changamoto za mikopo kwa akina mama hao

Dc kaminyoke ametoa maelekezo hay oleo may 8 2025 katika uzinduzi wa chemba ya wanawake wajasiriamali wilaya ya Bunda chini ya TANZANIA WOMEN CHEMBER OF COMARCE.

Sauti ya Mhe Aswege Enock Kaminyoge
Baadhi ya wanachama na wanufaika wa chemba TWCC

Baadhi ya wanachama na wanufaika wa chemba hiyo wamesema kuna fursa mbalimbali kwa wanawake kujiunga na umoja huo kutokana na kukutanishwa na wataalamu mbalimbali pamoja na taasisi za serikali zinazowapatia elimu ili kukabiliana na changamoto za kibiashara katika ujasiriamali wao

Aidha wametoa wito kwa wanawake wengine kutoogopa kujiunga na jukwaa hili kwa kuwa wapo walioanza pasipo kuwa na uelewa lakini hadi hivi sasa wametengeneza mtandao mkubwa wa biashara.

sauti ya wanufaika wa jukwaa la TWCC
Baadhi ya wajasiriamali waliojiungq na jukwaa la TWCC wakionesha walivyoongeza thamani Bidhaa zao

Kwa upande wake mkurugenzi wa jukwaa hili la TWCC Maria Isidory amesema tangu kuanzishwa kwa jukwaa hili mwaka 2005 limesaidia wanawake wengi katika kuhakikisha wanazifikia ndoto zao katika kuwasaidia elimu ya biashara, mitaji na kuwakutanisha na wataalamu pamoja na taasisi za serikali kama vile  TRA, SIDO miongoni mwa taasisi zingine

Sauti ya mkurugenzi wa jukwaa hili la TWCC Maria Isidory

No comments:

Post a Comment