Tulivundwe;Wanaotoa Mimba,kutupa watoto hii inawahusu.Bunda- Mara - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Tuesday 6 March 2018

Tulivundwe;Wanaotoa Mimba,kutupa watoto hii inawahusu.Bunda- Mara



Msanii wa nyimbo za asili  kutoka Nyanda za juu kusini Songwe mwenye masikani yake  Jijini Daressalaam  anayefahamika kama Tulivundwe Mwawalo ameachia wimbo  mpya  unaowataka wadada pamoja na wamama  kulea watoto.

Tulivundwe amesema hayo wakati  akiutamburisha wimbo wake mpya kwa wapenzi na wakazi wa kanda ya ziwa  unaokwenda kwa jina la Sungaga umwana  yaani tulee watoto uliosikika kupitia kipindi cha kwetu kwanza  ya 91.7 mazingira fm ambapo aliuachia kwa mara ya kwanza.

Akizungumzia  wimbo  huo ulioandaliwa  katika studio za Tivol zilizopo Jijini Mwanza  Tulivundwe amesema kuwa ametumia  lugha ya kinyiha,Kiswahili pia ameweka vionjo vya kisukuma katika wimbo huo ambapo amewaomba  mashabiki wake waupokee kwa mikono miwili.

Kwanza kabisa napenda kuwashukuru wenyeji wangu na wadau wote wa Bunda aah!  kitu ambacho naweza kusema kwamba nimewaletea nyimbo mpya  inaitwa Sungaga umwana naombeni muipokee kwa moyo na kwa upendo nawapenda sana na ndomaana nimeamua kuwafateni hadi huku Bunda.alisema Tulivundwe.

Tulivundwe ameachia wimbo huo uliobeba  ujumbe mzito kwa wale wenye tabia ya kutoa mimba pamoja na kutupa watoto wao wa kuwazaa ikiwa ni siku chache tu kufikia kilele cha maadhimisho ya  siku ya wanawake Dunia ambayo ufanyika march nane kwa kila mwaka.

Pia tulivundwe amewahi kutamba na vibao kama rafiki gani,tuilinde ngozi yetu,kasuku aliyomshirikisha Cos B sasa amekuja na Sungaga umwana ambapo amesema maandalizi ya video tayari yanaendelea.

Akizungumzia soko la muziki wa asili lilivyo kwa sasa tulivundwe amesema  vyombo  vya habari nchini bado vimeegemea kusuport muziki wa bongo fleva na kuwasahau wasanii wanaofanya muziki wa asili. 

Kitu ambacho nachojua kwa upande wangu mimi ni support kwa upande wa media upande wa radio wametusahau tunaofanya traditional wameegemea upande wa bongo fleva wamesahau muziki wa kwao ambao ni utamaduni wao lakini sisi wa muziki wa asili hatujapewa chance hatuna vipindi ambavyo vinapiga muziki wetu kwa mfano labda jumatano .alisema Tulivundwe.

Hata hivyo tulivundwe ameviomba vituo vya radio na tv nchini kutoa ushirikiano  kwa kusuport  kazi za wasanii wa muziki wa asili ili kufanya wasanii wa muziki huo kujulikana kitaifa na kimataifa akitolea mfano wa  waimbaji wa makhirikhiri  ambao  wamevuka boda kutokana na support kutoka kwao.

No comments:

Post a Comment