Bodaboda mjini Bunda kulipia leseni ya usafirishaji. - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Monday 5 March 2018

Bodaboda mjini Bunda kulipia leseni ya usafirishaji.

Waendesha bodaboda katika Wilaya ya Bunda Mkoani Mara wamepewa miezi miwili  kukata leseni ya usafirishaji abiria kabla serikali kuanza kuwachukulia hatua wale ambao watakuwa hawajatekeleza maelekezo hayo.
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa bunda Janeth Mayanja katika kikao kilichowakutanisha pamoja waendesha bodaboda, Jeshi la Polisi, ofisi ya mkuu wa wilaya pamoja na ofisi ya Sumatra mkoa Mara.
Aidha katika kikao hicho,Afisa Mfawidhi wa mamlaka ya udhibiti Usafiri wa nchi kavu na majini SUMATRA Mkoani Mara  Halima Lutavi  amewaeleza madereva hao kuwa leseni hizo wanapaswa kulipa kwa mujibu wa sheria lakini mjini bunda zoezi hilo limechelewa kuanza kutokana na kwamba imeanzishwa hivi karibuni, ambapo amesema kwamba leseni hizo zitatolewa na afisa biashara wa halmashauri ya mji wa bunda.
Hata hivyo Mkuu wa wilaya ya Bunda Mwl  Lydia Bupilipili  amesema lengo la serikali ni kutambua waendesha pikipiki maaarufu kama bodaboda na kuwawekea mazingira rafiki ili kunufaika na kazi zao.
Kwa upande wa madereva bodaboda wamesema kuwa wamepokea maelekezo ya serikali na wameahidi kuyafanyia kazi.

No comments:

Post a Comment