Mahafali kidato cha 4 Kabasa Sekondari ni Kambarage tena..!!!! - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Friday 6 October 2023

Mahafali kidato cha 4 Kabasa Sekondari ni Kambarage tena..!!!!


Ni katika Mahafali ya Kidato cha 4 shule ya Sekondari Kabasa, Kambarage Wasira akiwa mgeni rasmi atoa milioni 1 (1,000,000/=Tsh) kukabili sehemu ya changamoto katika shule hiyo.

Wahitimu wa kidato cha 4 Sekondari Kabasa wakifanya yao mbele ya wageni waalikwa.
Shangwe kama lote kwa walimu na wanafunzi Kabasa Sekondari
Miongoni mwa wageni waalikwa ilikuwa ni pamoja na walimu kutoka shule mbalimbali wilaya ya Bunda
Kambarage Wasira akizungumza katika mahafali ya 17 shule ya Sekondari Kabasa. Picha na Edward Lucas

Na Edward Lucas

Ikiwa ni wiki moja imepita tangu Kambarage ashiriki mahafali ya darasa la saba shule ya msingi Kunzugu na kutoa ahadi ya ‘Printa’ yenye thamani ya milioni 1 na laki 2 (1,200,000/=) hii leo ilikuwa ni zama ya Sekondari Kabasa akiwa mgeni rasmi tena.

Katika mahafali hayo, Kambarage Wasira ametoa shilingi milioni 1 ili kusaidia sehemu ya changamoto zinazoikabiri shule hiyo.

Sauti ya Kambarage Wasira
Godfrey Maige Maduhu, Mkuu wa shule ya Sekondari Kabasa. Picha na Edward Lucas

Awali akisoma taarifa ya shule, Mkuu wa shule hiyo, Godfrey Maige Maduhu amebainisha changamoto mbalimbali zinazoikabiri shule hiyo kuwa ni pamoja na ukosefu wa bwalo, maktaba, upungufu wa walimu na upungufu wa matundu ya choo 24 huku akiipongeza serikali ya awamu ya sita kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa kwani shule hiyo ina madarasa ya ziada 6

Sauti ya Godfrey Maige Maduhu
Grace Raymond akisoma risala ya wahitimu kidato cha 4 Sekondari Kabasa ikibainisha baadhi ya changamoto walizokumbana nazo
Sauti ya Grace Raymond

No comments:

Post a Comment