Nyamo-hanga azikwa leo kwao Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Wednesday, 16 April 2025

Nyamo-hanga azikwa leo kwao Bunda

 

Ni aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa TANESCO aliyefariki kwa ajali ya gari eneo la nyatwali Bunda

Na Adelinus Banenwa

Shughuli ya mazishi ya aliyekuwa mkurugenzi wa TANESCO Boniface Gissima Nyamo-hanga inaendelea nyumbani kwake Mtaa wa Migungani kata ya Bunda stoo Bunda mjini mkoani Mara .

Ibada ya Mazishi ikiongozwa na Askofu Mwita Maguge wa kanisa la kiinjiri la kirutheli Tanzania KKKT dayosisi mkoani Mara.

Katika ujumbe wake kwenye ibada hiyo askofu Mguge amesema hakuna mtu anayeweza kukikimbia kifo hata kama una ulinzi wa namna gani kifo kitakufuata.

Viongozi mbalimbali wamefika katika shughuli hizo zinaongozwa na Naibu waziri mkuu na waziri wa Nishati Mhe Dotto Biteko ambapo pia amesema tanesco na na taifa kwa ujumla limempoteza mtu muhimu sana ambaye mara zote alikuwa si mtu wa kulalamika bali akiona tatizo basi anatoa na njia ya kutatua tatizo hilo.

Akisoma wasifu wa marehemu Gissima Nyamo-hanga, Irene Gowele afisa mawasiliano TANESCO amesema Mhandisi Gissima alizaliwa tarehe 10 Sept 1969 mkoani Mara huku akishika nyadhifa mbalimbali za uongozi ikiwemo mkurugenzi mkuu wa REA  kati ya mwaka 2016 hadi 2019, wakala wa ujenzi Tanzania. TBA na baadae kuwa Mkurugenzi mtendaji wa TANESCO Tanzania ambapo hadi umauti alikuwa akitumika katika nafasi hiyo

Mhandisi Boniface Gissima Nyamo-hanga ameacha wajane wawili na watoto 15.

Ikumbukwe Mhandisi Nyamo-hanga alifariki dunia April 13, 2025 katika ajali ya gari eneo la Nyatwali Bunda

No comments:

Post a Comment