Dc Bunda atajwa na mwananchi kuwa ametoa rushwa asijadiliwe katika kamati ya siasa ya CCM - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Tuesday 16 January 2018

Dc Bunda atajwa na mwananchi kuwa ametoa rushwa asijadiliwe katika kamati ya siasa ya CCM



Zikiwa zimebaki siku tatu kuwasili kwa waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Majaliwa Kasimu  wilayani Bunda mkoani Mara kwa ziara ya siku mbili wilayani hapa,  mwananchi mmoja aliyejulikana kwa majina Bonphace Chacha amekamatwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuhusishwa na vitendo vya rushwa.
Akizungumza na waandishi  wa habari katika ofisi za chama cha mapinduzi CCM  mwenyekiti wa chama hicho Justine Rukaka ameeleza kwamba wameita jeshi la polisi pamoja  na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa takukuru wilayani hapa na kuwakabidhi mtuhumiwa huyo  kutokana na madai ya mazingira ya kuwepo viashiria vya vitendo vya rushwa  baina yake na mkuu wa wilaya ya Bunda mwl Lydia Bupilipili.
Mtuhumiwa huyo awali aliwekwa chini ya ulinzi na wajumbe wa kamati ya siasa ya chama hicho kilichoketi leo baada ya mtuhumiwa huyo  kuonana na mwenyekiti wa CCM  na kumweleza kwamba ametumwa na mkuu wa wilaya kuwa aongee na viongozi wa kamati hiyo ili  wasimjadili na anaomba msamaha kwa makosa aliyoyafanya.
Redio Mazingira fm  ilipotafutwa mkuu wa wilaya ya Bunda  kuthibitisha taarifa hizo amesema kuwa hajui chochote kuhusu madai hayo na hajamtuma mtu yeyote kumuombea msamaha ndani ya chama hicho.

Hata hivyo  ametoa onyo kwa wananchi kutokutumia jina lake vibaya kwani yeye anashughulikia matatizo ya wananchi hivyo wananchi waungane naye kuyatatua kwakuwa Bunda kuna matatizo mengi yanayotakiwa kushughulikiwa.

No comments:

Post a Comment