Mwalimu wa Shule ya Msingi Bigutu adakwa na wananchi baada ya kukutwa akiiba vifaa vya ujenzi shuleni Mjini Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Sunday 21 January 2018

Mwalimu wa Shule ya Msingi Bigutu adakwa na wananchi baada ya kukutwa akiiba vifaa vya ujenzi shuleni Mjini Bunda


 
Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Bigutu katika kata ya Bunda stoo hamashauri ya mji wa Bunda aliyejulikana kwa majina ya Said  MNEMA amekamatwa na wananchi kwa tuhuma za kukutwa Akiiba vifaa vya ujenzi wa shule hiyo vilivyochangwa kwa fedha za Wananchi.


Pendo Maguya ni mwananchi wa kata hiyo aliyeshuhudia mwalimu huyo akiiba sementi hatiamye kutoa taarifa kwa aliyekuwa mwenyekiti wa kitongoji hicho.

Amesema yeye pamoja na mwenzake Anastazia malagira walihisi kuwepo kwa uwizi katika vifaa hivyo vya ujenzi baada ya kuona mtu mmoja ambaye hawakumtaja jina mwenye toroli akisomba saruji kupeleka kwa mwalimu huyo.

Aidha Anastazi Malagira amesema ameshuhudia wizi wa sementi mifuko minne,Nondo na misumari,ambapo ameongeza kuwa walikuwa wanatoka kufata maji ndipo wakaona pikipiki na mtu mwenyetoroli akisimama katika mlango wa ofisi ya mwalimu mkuu na wakaamua kusubiri kuona kinachotoka ndani ya ofisi hiyo na kushuhudaia watu hao wakitoa vifa hivyo.

Naye kwa upande wake Makam mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo ameeleza kwamba amepata taarifa za wizi huo na kufika shuleni hapo ambapo alimkuta aliyekuwa mwenyekiti wa mtaa huo akiwa na mwalimu mkuu na alipomhoji mtuhumiwa huyoa alimweleza kuwa wakae wayamalize.
Hata hivyo Kaimu Afisa elimu wa shule ya msingi halmashauri ya mji huo Hundi Tanga Amesema kuwa amepata taarifa za tukio hilo na kuchukua hatua za kutoa taarifa polisi.

Diwani wa kata hiyo Chiruma Daud Subi ameeleza kwa amepata taarifa hizo na kufika katika eneo la tukio ambapo ameongeza kwamba baada ya ufuatiliaji wameshuudia matofari zaidi ya 300 pia zimehamishwa shuleni hapo na kupelekwa eneo analojenga mwalimu huyo anaetuhumiwa kwa wizi huo.

Hata hivyo Mkurugenzi wa mji wa Bunda Janeth Mayanja amelaani vikali tabia hiyo aliyoionyesha mwalimu huyo na kusema kuwa kwa upande wake atamchukulia hatua za kinidham kwani kitendo alichikifanya kinadidimiza jitihada za wananchi kuunga mkono serikali katika shughuli za kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment