Mkurungezi wa mamlaka ya Maji Bunda BUWASA asimamishwa kazi kupisha uchunguzi dhidi tuhuma zinazomkabili - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday 25 January 2018

Mkurungezi wa mamlaka ya Maji Bunda BUWASA asimamishwa kazi kupisha uchunguzi dhidi tuhuma zinazomkabili



Imeelezwa kuwa Mkurungezi wa Mamlaka ya maji Bunda BUWASA bwana Mansur Mandemula amesimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi kufuatia tuhumu zinazomkabili za kuwa na duka la vifaa vya huduma ya maji jambo ambalo ni kinyume.

Akizungumza na radio mazingira fm Kwanjia ya simu Mkuu wa Wilaya Ya Bunda Mwl.Lydia Bupilipili amethibitisha kusimamishwa kwa mkurungezi huyo na kwamba siku ya leo ndiyo amekabidhi ofisi ili kupisha uchunguzi.

Bipilipili amesema tayari bodi ya maji Imevunjwa kutokana na kuwepo kwa taarifa za kumtetea Mkurungezi huyo huku wakishindwa kutimiza wajibu wao kama bodi na badala yake wamesababisha hadi deni limefika milioni mia nne sabini na saba paka sasa hivi.

Aidha Bupilipili amesema kuwa awali aliwaeleza wajumbe wa bodi hiyo kuwa wao wapo kwajili ya wananchi na sio watu wengine na kwamba bodi ilionekana kutokuwa wabunifu katika kazi zao kwa wananchi.

Katika hatua nyingine Bupilipili amesema moja ya agizo la waziri mkuu ni kutuma wataalam kutoka Makao makuu TAMISEMI ili kuja kuchunguza miradi yote ya maji katika Wilaya ya Bunda ambapo tayari wataalam hao wameshafika na tayari wameshaanza kazi kama maagizo yalivyokuwa.

No comments:

Post a Comment