Kamishina wa TRA apewa siku 8 na Waziri Mkuu awe amempata mkandarasi aliyejenga jengo la TRA Sirari. - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Wednesday 17 January 2018

Kamishina wa TRA apewa siku 8 na Waziri Mkuu awe amempata mkandarasi aliyejenga jengo la TRA Sirari.


Waziri wa Tanzania Mh Kassim Majaliwa ametoa Siku 08 kwa Kamishena wa TRA kuhakikisha anamfikisha mkandarasi aliyehuska kujenga jengo la TRA Sirari ambapo ni mpakani mwa Tanzania na Kenya baada ya kutembelea eneo hilo na kutolidhishwa na ujenzi wake huku akienda na taarifa zote jinsi alivyokuwa akilipwa fedha hizo.

Hayo yamebainishwa leo mara baada ya Waziri kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Afya Sirari na kutembelea jingo hilo na kutoa kauli hiyo kuhusu ujezni wa jingo hilo la TRA Sirari mpakani mwa Nchi ya Kenya na Tanzania.
Awali waziri huyo ameweka jiwe la msingi katika  ujenzi wa kituo cha Afya Sirari baada ya Serikali kupeleka Millioni Miatano Mfuko wa Jimbo la Tarime vijiji  kupitia mbunge wake John Heche ukatoa Millioni Mianne na Wananchi kuchangia Millioni Mianne Waziri huyo naye aklachangia Millioni Miatano ili kuongeza Ngunvu na kusema kuwa Serikali nayo inatoa Shilingi millioni Miambili Themanini kwa ajili ya ununuzi waVifaa huku akipongeza ujenzi wa kituo hicho cha Afya.

Pia Waziri amesema kuwa serikali itawachukulia hatua kali wale wanaendelea kukatisha ndoto za watoto wa kike hapa Nchini.

Aidha Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijiji CHADEMA John Heche akaomba Waziri kuruhusu uuzaji wa nafaka yakiwemo mahindi Nchi jirani ya Kenya huku Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Esther Matiko CHADEMA akiwapongeza wananchi wa Sirari kwa kujitoa katika ujenzi wa Kituo cha Afya na kuomba Serikali kuendelea kuwaunga Mkono wanachi katika ujenzi wa Miundombinu ya Afya naElimu.

Waziri Mkuu bado anaendelea na ziara yake Mkoani Mara ambapo kwa sasa bado yuko Wilayani Tarime na ataelekea Serengeti baada ya kuongea na wakazi wa Nyamongo Kesho.


No comments:

Post a Comment