Hatua za haraka zaanza kuchukuliwa kuondoa adha ya ukosefu wa choo Shule ya Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Friday 26 January 2018

Hatua za haraka zaanza kuchukuliwa kuondoa adha ya ukosefu wa choo Shule ya Bunda




Wanafunzi,Waalimu pamoja na wakazi wanaofanya shughuli zao katika shule ya Msingi Bunda halmashauri ya mji wa Bunda Mkoani Mara wako hatarini kupatwa na Magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu kutokana na shule hiyo kukosa choo jambo linalowalazimu wanafunzi pamoja na walimu kujisaidia mlimani.

Taarifa zinaeleza kwamba wanafunzi wa darasa la awali yaani chekechea,la kwanza, la pili na hata madarasa mengine baadhi yao hulazimika kuchimba mchanga kwa mikono katika eneo la uwanja wa mpira wa miguu shuleni hapo kisha hujisaidia haja kubwa na baadae huyafunika.

Alipoulizwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji huo Janeth Mayanja amesema kuwa suala hilo la ukosefu analitambua na tayari wameanza kulishughulikia kwa kujenga choo cha dharura kwa wanafunzi hao ikiwa sambamba na ujenzi wa matundu 16 ya vyoo vya kudumu.

Taarifa kutoka katika shule hiyo zinadai kwamba leo wameanza uchimbaji wa matundu hayo ya vyoo.

Hata hivyo wananchi wameshukuru redio mazingira fm  pamoja na serikali ya mji wa bunda chini ya mkurugenzi wake Janeth Mayanja  kwa hatua alizozichukua katika kunusuru adha hiyo .

No comments:

Post a Comment