Kompashen ya Kanisa la ANGILKAN Mjini Bunda imesaidia kupunguza wimbi la watoto wa mitaani- FLAVIAN JOSEPH NYAMIGEKO - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Wednesday 21 February 2018

Kompashen ya Kanisa la ANGILKAN Mjini Bunda imesaidia kupunguza wimbi la watoto wa mitaani- FLAVIAN JOSEPH NYAMIGEKO



MWENYEKITI wa kamati ya Watoto Katika kompasheni Kanisa la ANGILKAN Mjini Bunda Mkoani Mara Bwana FLAVIAN JOSEPH NYAMIGEKO amesema huduma zanazitolewa na kompashen hiyo imesaidia kupunguza wimbi la watoto wa mitaani mjini halo. 

Amesema Katika Kanisa lao la ANGILKAN kupitia kompashen hiyo inalea jumla ya watoto 296 wanaolewa mahitaji yote muhimu za kibinadamu.
Bwana Flavian ameeleza kuwa pamoja na kuepusha madhila ya uwepo wa watoto wa mitaani lakini wao jukumu lao ni kuwasimamia watoto hao hadi pale watakapo jimudu kimaisha. 

Ameeleza huduma wanazopewa watoto hao ni pamoja na kuwasomesha, kuwapatia huduma ya afya pindi wanapougua pamoja na kuwapatia nyenzo za kuendeshea Maisha wawapo katika hatua za kujitegemea.

Hata hivyo amewaomba wananchi kuwathamini watoto wanaishi Katika mazingira magumu kwani wao ni watu  na wanapaswa kupatiwa huduma kama watu wengine na kuongeza kuwa katika mtihani wa kidato cha nne yaliyotolewa matokeo hivi karibuni jumla ya watoto 28 wamefaulu wanaosimamiwa na Compashen.

No comments:

Post a Comment