Bupilipili awaongoza UVCCM Wilaya ya Bunda katika ushiriki wa ujenzi wa kituo cha Afya Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Wednesday 28 February 2018

Bupilipili awaongoza UVCCM Wilaya ya Bunda katika ushiriki wa ujenzi wa kituo cha Afya Bunda



Umoja vijana wa chama cha mapinduzi uvccm wilaya ya Bunda mkoani Mara chini ya mwenyekiti wake gasper Charles wameshiriki kutoa msaada wa kusaidia ujenzi katika kituo cha afya bunda kinacho jengwa katika kata ya Kabarimu.

Akizungumza na vyombo vya habari katika eneo la ujenzi wa kituo hicho cha afya Bwana Gasper amesema kuwa katika kusimamia ilani ya chama cha mapinduzi wameamu kuungana na viongozi wa chama hicho katika ujenzi huo kwa maslahi mapana ya wananchi pamoja na kumsaidia rais john pombe magufuli kusimamia miradi ya maendeleo inayoendelea nchini.

Naye katibu wa umoja huo shija steven amewaomba vijana mjini bunda kutumia miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali kujipatia ajira badala ya kukaa vijiweni bila kazi.

Hata hivyo katika kusaidia ujenzi wa kituo hicho mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Bunda ambae pia ni mkuu wa wilaya Mwl. Lydia Bupilipili ameshirikiana na vijana hao katika kuhakikisha ujenzi wa kituo hicho kilichotolewa fhedha shilingimilioni mia tano inakamilika kwa ufanisi wa hali ya juu , pia amewapongeza vijana wa umoja wa chama hicho katika kuonyesha uzalendo wa kweli.

No comments:

Post a Comment