Tunashangazwa! wahalifu kuachiwa huru_Bunda Mara - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Wednesday 21 February 2018

Tunashangazwa! wahalifu kuachiwa huru_Bunda Mara



Wananchi katika kata ya Balili halmashauri ya mji wa Bunda Mkoani Mara Wameiomba serikali kuwakubalia wananchi kuwaadhibu  wahalifu.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katani hapo Petro Nyamagaka mkazi wa eneo hilo amedai kuwa anashangazwa na hatua ya jeshi la polisi kuwazuia wananchi kumuadhibu mwizi kwani ilhali anapofikishwa kituo cha polisi badae huachwa huru.

Amesema kitendo cha kuaachia huru huongeza hofu kwa wananchi na wakati mwingine huwapa nguvu wahalifu kuendelea na vitendo viovu katika jamii.

Kwa upande wake afisa polisi kata amewahakikishia wakazi wa mtaa wa rubana na kata ya balili kiujumla kwamba mhalifu akifikishwa jeshi la polisi na wananchi wakatoa ushahidi hatua za kisheria hutekeleza kama kawaida.

Aidha ameeleza kwamba changamoto inayosababisha wahalifu hao wanaachwa ni pale ushaidi unapokosekana, na kuwasihi wananchi kutoa ushirikiano pindi wanapotakiwa kufanya hivyo ili haki itendeke.

Naye Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ambae pia ni Mtendaji wa kata hiyo Bwana Thomas Bure amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola katika masuala ya ulinzi na usalama ili kupunguza vitendo viovu katika maeneo yao.

Amesema wakati huu ambapo wananchi wengi wamelima zao la pamba na wanategemea kupata pesa nyingi nidhahiri kuwa wezi wataongezeka kwahiyo wanatakiwa kuunda vikundi vya ulinzi vitakavyosaidia kudhibiti wizi na uporajimdogomdogo.

Bwana Bure ameeleza kwamba wakati watakapounda hivyo vikundi jeshi la polisi litawapatia mafunzo ya namna bora ya kukamata wahalifu .

Hata hivyo ametoa wito kwa wakazi hao kufuata sheria badala ya kujichukulia sheria mkononi kwakuwa kufanya hivyo ni kwenda kinyume na utaratibu wa nchi na atakayefanya hivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.


No comments:

Post a Comment