Bitaraguru waomba zahanati yao ifunguliwe ianze kutoa huduma kwa wananchi-Bunda Mara - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Tuesday 20 February 2018

Bitaraguru waomba zahanati yao ifunguliwe ianze kutoa huduma kwa wananchi-Bunda Mara


Wananchi katika kijiji cha Bitaraguru kata ya Kabasa Halmashauri ya mji wa Bunda Mkoani Mara wameiomba serikali iwefungulie zahanati ya bitaraguru ambayo kwa sasa haitoi huduma kwa wananchi licha ya kuonekana kukamilika.

Ombi hilo limetolewa na wananchi hao kupitia kipindi cha Duru za Habari kinachorushwa na kituo hiki baada ya kufika eneo hilo kuzungumza na wananchi kuhusu maoni yao jinsi walivyopokea mradi huo mkubwa ambao unaonekana kukamilika.

IMELDA BWIRE pamoja na LETICIA JOSEPHAT wamesema kuwa ni muda sasa hawaoni zahanati hiyo inaanza kutoa huduma licha ya wao kuona imekamilika.

Aidha wamesema watafurahi  sana siku ambayo zahanati hiyo itaanza kutoa huduma kwa wananchi kwani itakuwa imewasaidia sehemu kubwa katika shida walizokuwa wanazipata kama wananchi wa eneo hilo.

Naye PAULO KASERA ambaye ni mmoja ya viongozi kutoka kijiji hicho amesema kuwa serikali ya kijiji inafuatilia kuuliza kuhusu kufunguliwa kwa zahanati hiyo wanaambiwa kuwa zahanati hiyo haijafikia kufunguliwa maana bado haijasajiliwa.
Katika juhudi za kumtafuta mganga mkuu wa Halmashauri ya mji wa Bunda ili kupata ufafanuzi wa suala hilo bado zinaendelea.

No comments:

Post a Comment