Kutoka uwanja wa taifa; simba (tanzania) 4-0 gendamarie (djibouti) ....(full time) - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Sunday 11 February 2018

Kutoka uwanja wa taifa; simba (tanzania) 4-0 gendamarie (djibouti) ....(full time)

MPIRA UMEKWISHAAAAAA
DAKIKA 3 ZA NYONGEZA
GOOOOOOOO Dk 90, Okwi anaandika bao safi kwa mkwaju mkali wa mpira wa adhabu aliosetiwa
Dk 89 kipa yuko chini akiwa hajaguswa na mtu, inaonekana ni lengo la kupunguza mabao zaidi


Dk 86 Bocco anamtoka beki lakini anawahi kuokoa na kuwa kona, inachongwa vizuri lakini Kotei anaukosa
Dk 84 kona safi inachongwa, Kazimoto anaachia mkwaju, hakuna kitu
Dk  83, Okwi anaachia mkwaju mkali, kipa anaokoa, konaaa
DK 82, Simba wanagongeana vizuri lakini wanashindwa kuipasua ngome ya GEndamarie
SUB Dk 81 Mogel anakwenda nje upande wa Gendamarie anaingia Aden
Dk 79, Kapombe anaachia mkwaju mkali sana, lakini hakulenga lango...goal kick
Dk  76 mkwaju mkali wa adhabu wa Okwi, unamgonga mchezaji wa Simba unakwenda nje, goal kick


SUB Dk 75, Ndemla anakwenda benchi upande wa Simba na nafasi yake inachukuliwa na mkongwe Mwinyi Kazimoto
SUB Dk 72, Simba wanamtoa Kichuya na nafasi yake inachukuliwa na Muzamiru
Dk 69 kiasi fulani wanaanza kucheza lakini wanatumia mbinu ya kujiangusha kupoteza muda
Dk 66, Simba wanaingia vizuri kabisa, krosi ya Bocco inampoteza Okwi
Dk 65 sasa, mchezaji mmoja wa Gendamarie yuko chini anatibiwa 
Dk 61 Simba inapata kona baada ya shuti la Asante kuguswa na kwenda nje, inachongwa kona fupi, haina matunda
Dk 59, Ndemla anaachia mkwaju mkali kabisa hapa lakini kipa yuko vizuri, anaokoa kwa ustadi mkubwa
SUB Dk 58 Yabeh Idriss anaingia kuchukua nafasi ya Hussein aliyekosa penalti


SUB Dk 55 Ismail anatoka anaingia Osman Mohammed upande wa Gendamarie
Dk 53, krosi nzuri ya Bocco lakini mpira wa Okwi unatoka nje, pasi ilikwenda nyuma yake
Dk 51 Okwi anaingia vizuri ndani ya eneo la Gendamarie, konaaaaaa, inachongwa, Gendamarie wanaokoaa
Dk 50, inapigwa Manula anapangua vizuri kabisa hapa 
PENATAAAAAATT Dk 50 Gendamarie wanapata penalti baada ya mshambuliaji kuanguka ndani ya eneo la hatari
Dk 47 Kwasi anaingia na kuachia mkwaju safi wa krosi lakini ni laini kabisa 
Dk 45 Mpira umeanza na kasi na Simba wanaonekana wanataka kuendelea kutupia mabao




MAPUMZIKO
DAKIKA 2 ZA NYONGEZA
GOOOOOOOO Dk 45, Bocco anaruka na kupiga kichwa kinakwenda moja kwa moja wavuni
Dk 44, Abdallah anapiga shuti upande Gendamarie
Dk 42, Simba wanapata nafasi nyingine tena, lakini inaonekana bado hawako makini
Dk 39 krosi safi ya Bocco, Kichuya anachelewa na kushindwa kuunganisha
Dk 37, Simba wanaendelea kusmbulia mfulilizo lakini kipa wa Gendamarie ni kizingiti
GOOOOOOOOO Dk 33 Bocco anaruka na kupiga kichwa kinachojaa wavuni moja kwa moja. Ni baada ya tokea piga nikupige kwenye lango la Gendamarie

Dk 30, Simba wanaendelea kushambulia mfululizo huku wakipoteza mipira mingi
Dk 27 ndani ya dakika 2 Simba wameotea mara tatu na hili nalo wanapaswa kuliangalia kwa muda muda unasonga mbele na Gendamarie wangependa kama ni kupoteza basi kwa idadi ndogo ya mabao


Dk 26 sasa, ikiwezekana Simba wanaweza kubadilisha aina ya pasi nyingi za mwisho, badala ya ndefu wakatumia fupi. Kwani ndefu nyingi hasa za juu zimekuwa zikipotea
Dk 22, Asante anaruka juu na kupiga kichwa lakini kipa anaonyesha wamo, anadaka vizuri kabisa
Dk 20, krosi nzuri kabisa lakini Kapombe anaruka na kupiga kichwa juuuuu
Dk 19, Kichuya anaachia mkwaju, konaaa. Inachongwa lakini Gendamarie wanaokoa hapa
Dk 17 Okwi anaingia vizuri, ajajaribu lakini kipa yuko makini
Dk 15 Simba wanapata kona lakini haikuwa na matunda
Dk 11, Gendamarie bado wanaendelea kubaki kwenye upande wao kuhakikisha wanajilinda vilivyo
Dk 8, Bocco anaruka juu na kupiga kichwa, goal kick. 


Alikuwa mwenyewe, angetulia, angeandika bao la pili
Dk 8, Gendamarie inafanya shambulizi la kwanza, goal kick
Dk 7, hali ilivyo, inaonekana Gendamarie wameweka watu 9 nyuma ya mpira
Dk 6, Simba wanapata kona baada ya mpira kuzuiliwa
GOOOOOOOOO Dk 2, Ndemla anafunga bao safi kwa mkwaju wa adhabu
Dk 1, Bocco anawekwa chini nje kidogo ya lango la Gendamarie
Dk 1, mechi imeanza na Simba ndiyo wanaoanza mpira kusukuma mashambulizi upande wa Gendamarie

No comments:

Post a Comment