Ombeeni Taifa bila kukoma-Mchungaji Frederick Jumanne Bunda Mara - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Monday 19 February 2018

Ombeeni Taifa bila kukoma-Mchungaji Frederick Jumanne Bunda Mara



Watanzania Katika Wilaya Bunda Mkoani Mara wametakiwa kuacha siasa makanisani bali waendelea kuliombea taifa pamoja na viongozi wake bila kukoma ili amani na utulivu uendelee kuwepo siku zote katika taifa la Tanzania.

Rai hiyo imetolewa na Mtumishi wa Mungu Mchungaji Frederick Jumanne katika ibada takatifu siku ya jumapili katika kanisa la E.A.G.T  Chiringe Mjini Bunda ambapo alisema siku hizi siasa imeingia hadi kanisani katika hali ambayo hata waamini wanashindwa kuelewa kinachoendelea makanisani.

Jumanne amesema ni bora watanzania hasa waliowatumishi wa Mungu wakatumia muda wao gi kuliombea taifa na sio kujiingiza katika mambo ya siasa kwani kufanya hivyo ni kusahau majukumu uliyopewa kama mtumishi.

Jumanne amesema maombi ni silaha kubwa katika kumshinda adua yako hivyo watanaznia wajikite katika maombi ili adui wa Taifa la Tanzania akapata kushindwa.

No comments:

Post a Comment