Wananchi watakiwa kujitokeza kupima afya zao _Bunda Mara - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Wednesday 21 February 2018

Wananchi watakiwa kujitokeza kupima afya zao _Bunda Mara

Wito umetolewa kwa wananchi wilayani Bunda Mkoani Mara kujitokeza kwa kwingi kupima afya kwani ni njia moja wapo  ambayo mtu inamweka huru kama akijuwa maendeleo ya afya yake.

Wito huo umetolewa na  Mratibu  wa shughuli  za UKIMWI  katika halmashauri ya wilaya ya Bunda mkoani  Mara, Vitus  Gwanko wakati akizungumza na Radio Mazingira fm ofisini kwake wakati akitolea ufafanuzi yale yaliojiri kwenye baraza la madiwani hivi karibu katika kile alichokisema katika kikao hicho juu ya serikali  kutokuwa na bajeti kwa sasa  ya  kuwahudumia wananchi  wa kawaida wanaoishi  na virusi  vya UKIMWI badala yake  shughuli hiyo imeachiwa  mashirika yasiyo ya kiserikali(NGO’s).

Gwanko amesema kuwa kwa mwongozo waliyo nayo  sasa halmashauri  imeweka bajeti  ya  kuwahudumia  watumishi  wa umma pekee  wanaoishi  na VVU  ndani  ya  halmashauri husika na sio watu wa kawaida.

Kwa mujibu  wa Gwanko, halmashauri ya wilaya ya Bunda kwa sasa haina bajeti  ya kuwahudumia waviu, ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa wananchi  juu ya UKIMWI, upatikanaji  wa madawa  ya ARV’s na huduma zingine.

No comments:

Post a Comment