Waturuki nao walikuwepo uwanja wa taifa kuiunga mkono simba ikiitwanga gendamarie mabao 4 - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Sunday 11 February 2018

Waturuki nao walikuwepo uwanja wa taifa kuiunga mkono simba ikiitwanga gendamarie mabao 4




Baadhi ya raia wa Uturuki wanaoishi nchini, wametua kwenye Uwanja wa Taifa kuisapoti Simba iliyokuwa ikiivaa Gendamarie ya Djibouti.

Simba ilikuwa ikiivaa timu hiyo katika mechi yake ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika na kushinda kwa mabao 4-0.

Mashabiki hao wakiwa na bendera ya nchi yao, muda wote walikuwa wakiishangilia Simba kwa nguvu.


Hivi karibuni, Simba walitembelea ubalozi wa Uturuki nchini kwa mwaliko wa balozi na kupata chakula cha usiku, pamoja.

Mabao ya Simba katika mchezo huo yamefungwa na Said Ndemla, John Bocco aliyepiga mawili na Emmanuel Okwi aliyepiga msumari wa mwisho.

No comments:

Post a Comment