Makonda kupitia upya taaluma za wanasheria, asimamisha kesi zote - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Saturday 10 February 2018

Makonda kupitia upya taaluma za wanasheria, asimamisha kesi zote


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amesimamisha shughuli zote za mabaraza ya kata mkoani humo pamoja na kesi zote hadi hapo utaratibu wa kupitia upya taaluma za wanasheria waliopo katika mabaraza hayo utakapofanyika.
Makonda ameeleza kuwa wengi hawawezi kazi ndio maana wanashindwa kutatua migogoro ya ardhi na kusababisha Serikali kulaumiwa na wananchi.
Makonda ametoa kauli hiyo leo katika ukumbi wa Diamond Jubilee katika mkutano wa kupokea taarifa za malalamiko ya wananchi yaliyowasilishwa kwa wanasheria wa mkoa huo.
Makonda amewataka makatibu wa tarafa wote kuanzia Februari 12, mwaka huu kuanza kutembelea mabaraza hayo.

No comments:

Post a Comment