Mzee Mwinyi Afuta Kauli yake - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Monday 12 February 2018

Mzee Mwinyi Afuta Kauli yake




Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi amekiri kufuta kauli yake iliyodumu kwa takribani miaka 30 kuwa Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu na haitakaa ifanye vizuri kwenye michezo.

Mwinyi ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya awali kati ya Simba SC dhidi ya Gendarmerie ya Djibouti, baada ya mchezo alisema kiwango cha mpira nchini kwasasa kimekua hivyo anafuta kauli yake.
 
Katika mchezo wa jana Simba SC iliibuka na ushindi wa mabao 4-0 hivyo kujiweka vizuri kwenye mchezo wake wa marudiano huko Djibouti. Yanga pia ilishinda dhidi ya St. Louis ya Shelisheli.

Yanga inayocheza klabu bingwa Africa itasafiri kwenda Shelisheli kwaajili ya mchezo wake wa marudiano Februari 20 huku Simba inayoshiriki Kombe la Shirikisho nayo itasafiri kuelekea Djibouti kwaajili ya mchezo wa Februari 20 au 21.

No comments:

Post a Comment