Hospitali ya Manyamanyama iliyopo katika halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara jana jumatatu imepokea vitanda ,magodoro pamoja na mashuka yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni kumi na nane viliyotolewa na Rais wa Tanzania kupitia wizara ya afya na kukabidhiwa hospitalini hapo na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mara Agness Marwa.
Akizungumza wakati wa
kukabidhi vitanda hivyo
mbunge wa viti maalum mkoa wa
Mara kupitia tiketi ya CCM Agness Marwa
ambae pia amekuwa mgeni rasmi katika zoezi hilo amesema kuwa anamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr.John
Pombe Magufuri kwakutoa vifaa hivyo kupitia
wizara ya afya hivyo kufanya huduma katika hospitali za serikali kuendelea kuwa
bora zaidi.
Bi.Agness
amekabidhi hospitalini hapo vitanda vya kawaida ishirini,vitanda vya kuzalia vitano,magodoro
ishirini na mashuka hamsini vyenye
thamani ya zaidi ya shilingi milioni kumi na nane ambapo amesema kuwa tayari
serikali imetoa milioni mia tano kwa ajiri ya ukarabati wa majengo hospitalini hapo kwa lengo la kuokoa vifo vya
wakinamama na watoto.
Naye mganga mkuu wa
halmashauri ya mji wa Bunda dr.Nikodemasi nikorausi Masosota amempongeza
raisi Magufuri kwa kuyaona matatizo ya watanzania hasa wakinamama na
watoto ambao walikuwa wanalala chini
hivyo kuona umuhimu wa kusambaza vitanda
kwa kila halmashauri hapa nchini kwani idara ya afya imekuwa nachangamoto
nyingi nchini .
No comments:
Post a Comment