Wazazi wamkataa mkuu wa shule ya Nansimo kwa madai ya kutafuna fedha zao>Bunda Mara - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Sunday 25 February 2018

Wazazi wamkataa mkuu wa shule ya Nansimo kwa madai ya kutafuna fedha zao>Bunda Mara

Wakazi wa kijiji cha Nansimo katika halmashauri ya wilaya ya bunda mkoani Mara wamemkataa Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Nansimo kwa madai ya kutafuna fedha za michango ya wazazi waliyotoa kwaajili ya kulipa waalimu wa kujitolea.
Wakizungumza katika mkutano wa shule na wazazi kilichoketi shuleni hapo wazazi hao wameonyesha kutoridhishwa na namna fedha walizochanga zinavyotumika kuwalipa walimu hao huku wakieleza kwamba taarifa wanazopewa ya malipo ya walimu ni tofauti na hali halisi.
Akitoa ufafanuzi wa madai hayo Mwalimu mkuu wa shule hiyo elias Supira ameeleza kwamba taarifa walizo nazo wazai ni batili kwakuwa walimu hao wanalipwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa mkataba.
Naye mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya kata ambae pia ni diwani wa kata hiyo bwana sabato mafwimbo amesema kwamba anaheshimu mawazo ya wananchi lakini mwenye maamuzi ya kumuhamisha mwalimu ni mkurugenzi wa halmashauri.

No comments:

Post a Comment