Wazazi katika mji wa Bunda washauriwa kuwekeza kwa Vijana wao kupitia ufundi - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Saturday 23 December 2017

Wazazi katika mji wa Bunda washauriwa kuwekeza kwa Vijana wao kupitia ufundi

Wazazi na walezi katika halmashauri ya mji wa Bunda Mkoa wa Mara,wameaswa kuwafundisha vijana wao kazi za mikono za kujiajiri ili waweze kujikimu pindi wakati ukifika wa kujitengemea wasipate shida.

Hayo yamesemwa na Bwile Chisumu mkazi wa kata ya kabarimu mjini hapa wakati akizungumza na radio Mazingira fm  ambaye anajishughurisha na useremala na kueleza kuwa endapo wazazi wakianza kuwafundisha vijana wao kazi za ufundi itawasaidia pindi wakijitegemea na kuacha kutegemea kusubili ajira kutoka serikalini.


Chisumu ameongeza kuwa imefika wakati sasa kwa kila mwananchi kutambua kuwa kufanya kazi ni muhimu kwa kila mtu  na kutochagua wala kuidharau kazi kwa misingi fulangi kwani kazi nzuri ni yeyote inayokupatia kipato halali. 

No comments:

Post a Comment