Wafugaji wa Kata ya Bunda stoo wako vizuri katika kutekeleza maagizo ya serikali - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Sunday 24 December 2017

Wafugaji wa Kata ya Bunda stoo wako vizuri katika kutekeleza maagizo ya serikali

Jumla ya ng’ombe 7485 katika kata ya bunda stoo katika halmashauri ya mji wa bunda  imesajiliwa ikiwa ni sambamba na uwekaji  chapa zoezi lililochukua siku 10 kukamilika.

Zoezi hilo la uwekaji chapa kwa mifugo lilianzia katika kijiji cha butakale.

Akisoma taarifa fupi ya mifugo mbela ya mkuu wa wilaya ya Bunda, mtendaji wa kata hiyo bwana  Raymond Bukombe amesema kuwa kata hiyo inajumla ya mifugo 27485 na yote imesajiliwa.


Hata hivyo mkuu wa wilaya ya bunda Mwalimu Lydia Bupilipili amewapongeza wafugaji wa kata ya bunda stoo kwa kuhamasika kepeleka mifugo yao kuwekewa chapa na kusajiliwa kwa kuwa zoezi hilo ni la kitaifa na ni muhimu kwani inapunguza baadhi ya changamoto ikiwemo wizi wa mifugo

No comments:

Post a Comment