Barabara bado ni changamoto katika kijiji cha Ruamkoma Wilayani Butiama - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Saturday 23 December 2017

Barabara bado ni changamoto katika kijiji cha Ruamkoma Wilayani Butiama


Wananchi wa kijiji cha  Ruamkoma kata ya Butiama Wilaya ya Butiama  mkoani  Mara wameiomba serikali kuwaboreshea miundombinu ya barabara katika kijiji hicho kwani wamekuwa wakishidwa kufanya shughuli za kimaendeleo katika kijiji hicho.

Hayo yamesemwa na wananchi wa kijiji wa ruamkoma wakati wakizungumza na mazingira fm kwa nyakati tofauti.

Mwikwabe Marwa ambae ni miongoni mwa wananchi hoa amesema kuwa wamekuwa wakipata shida kubwa ya kusafirisha bidhaa zao za biashara kutokana na ubovu wa barabara zilizopo katika kata hiyo na kuwalazimu kutumia gharama kubwa wakati wanapokuwa wanasafirisha bidhaa zao.


Aidha wamesema changamoto zingine wanazokumbana nazo ni pamoja na maji, umeme, na upungufu wa vyumba vya madarasa ya shule ya msingi na kuomba serikali kuwapelekea huduma hizo.

No comments:

Post a Comment