Mgambo wapongezwa na mkuu wa wilaya ya Bunda kwa kujitokeza kwao kwenye mafunzo - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Sunday 24 December 2017

Mgambo wapongezwa na mkuu wa wilaya ya Bunda kwa kujitokeza kwao kwenye mafunzo

Mkuu wa wilaya ya Bunda Mkoani Mara mwl.Lydia Bupilipili amewapongeza wale wote waliojitokeza miaka ya nyuma kushiriki mafunzo ya mgambo, kwani wamekuwa msaada mkubwa ndani ya jamii katika utekelezaji wa majukumu ya ujenzi wa taifa.

Bulipili ametoa Pongezi hizo siku chache baada ya wanamgambo 166 kuchukuliwa na Suma jkt, kwajili ya kwenda kulinda katika makampuni  mbalimbali hapa nchini.

Aidha Bulipili amesema kuwa, vijana waendelee kujitokeza kwa wingi kushiriki mgambo kwani serikali ya wilayani Bunda imedhamilia kumaliza kero mbalimbali likiwemo suala la ajira. 

Hata hivyo Bupilipili  amesema mngambo ni kitu muhimu sana na sio cha kubezwa hata mara moja hivyo vijana wasione aibu kushiriki kwa asilimia mia moja.




No comments:

Post a Comment