Suala la Pembejeo feki wilayani Bunda kupatiwa majawabu. - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday 21 December 2017

Suala la Pembejeo feki wilayani Bunda kupatiwa majawabu.

Taasisi za serikali pamoja na taasisi Binafsi katika Wilaya ya Bunda Mkoani Mara wametakiwa kusimamia ipasavyo suala la pembejeo zinazotakiwa kuwafikia wa wakulima ili kuwawezesha kulima kilimo bora na sio bora kilimo.

Agizo hilo limetolewa Jana na Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mwalimu Lydia Bupilipili wakati akifungua wa mdahalo kuhusu Pembejeo feki Wilayani Bunda ulioandaliwa na Baraza la kilimo na mifugo Tanzania |Agricultural Council of Tanzania ] katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Bupilipili amesema Taasisi zinazohusika na usimamizi wa pembejeo wasipokuwa makini siku zote wataendelea kutiwa doa na wale wasiowatakia meme katika kazi yao hivyo amewataka kuamka nakuona sasa si muda wakufumbia macho masuala kama hayo.

Bupilipili amesema Wilaya ya Bunda inaongoza kwa pembejeo feki hivyo kuna kila sababu ya kuwa makini na watu wasio takia mema taifa lao kupitia kusambaza pembejeo feki kwa wakulima.


Bwana Khalid Ngassa kutoka Baraza La kilimo na mifugo Tanzania kwa upande wake amesema kuwa wakulima wanapata hasara kubwa na wanaumia sana kupitia pembejeo feki wanazopokea kutoka kwa wasambazaji hali ambayop inapelekea wakulima kukata tamaa na kilimo hivyo ameshauri wakulima nao wawe makini na pembejeo hizo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa mapema kama wakigundua kunadosari popote.

Kwa upande wao wakulima wa Wilaya Bunda wamekubalia kwa kauli moja ya kufuata ushauri waliopewa ikiwa ni pamoja na kusema pale ambapo kuna kasoro ili wawahi kusaidiwa tatizo hilo.

No comments:

Post a Comment