Mwanafunzi amejikuta akiingia katika ulimwengu mpya baada ya kubakwa na Baba mdogo wake ambaye ndiye mlezi wilayani Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Tuesday 19 December 2017

Mwanafunzi amejikuta akiingia katika ulimwengu mpya baada ya kubakwa na Baba mdogo wake ambaye ndiye mlezi wilayani Bunda

Sasu  (si jina lake halisi) ni mwanafunzi wa Darasa la sita katika shule moja ya msingi iliyoko Wilayani Bunda mkoani Mara.
Mwanafunzi huyo alijikuta akiingia katika ulimwengu mpya baada ya kubakwa na Baba mdogo wake ambaye ndiye mlezi wa mtoto huyo tarehe 12 ya mwezi wa 12 mwaka 2016  wakati akiwa darasa la tano.
Baba mdogo alimchukua ili amlee wakati akiwa bado ni mdogo.
Kulingana na mwanafunzi huyo, Baba yake mdogo huyo mwenye wake wawili alianza kumfanyia kitendo hicho chA kinyama akiwa darasa la tano.
Kulingana na mwanafunzi huyo, mara kwa mara Baba mdogo huyo ambaye kwa wakati huo alikwa amemzidi umri kwa miaka kama 48, alimwimuita katika nyumba yake pindi walipo baki wawili nyumbani na kumlazimisha kufanya tendo hilo huku akimtishia kumuua endapo atasema kwa watu.
Baba huyo alizoea kumfanyia kitendo hicho hali ambayo iliendea kumuumiza mwanafunzi huyo na ndipo alipoamua kufanya maamuzi ya kusema kwa walimu wake wa hapo shuleni lakini walimu wao wakadhani ni kama utani kulingana na maneno ya wanafunzi huyo.
“Alikuwa akiniambia nilale chini halafu ananivua nguo na kujaribu kuingiza uume wake kwangu…lakini nilikuwa naumia .alisema mwanafunzi



Lakini siku moja walimu wa shule hiyo waliamini maneno ya wafunzi huyo baada ya kuonyesha hisia za kuumizwa na kitendo hicho ndipo nao wakaamua kumfikishia taarifa mwalimu mkuu wa shule hiyo ili watafute ufumbuzi wa suala hilo.
 “Sisi walimu tulichokifanya nikwenda kwa mkuu wetu wa shule lengo nikuona mwanafunzi wetu anasaidiwa” walisema walimu
Mwalimu mkuu alisema alichokifanya aliwaita viongozi akiwemo na mwenyekiti wa kamati ya shule ,Mwenyekiti wa kijiji,na wajumbe baadhi wa kamati ya shule ili kuwapa taarifa hiyo.
 “Mimi nilichofanya nilimuuita mwenyekiti wangu wa kamati ya shule na mwenyekiti ya kijiji pamoja na wajumbe wa kamati nikawambia wao wakaamua kwenda na mwanafunzi Hospital pamoja kituo cha polisi lakini baada ya hapo mimi sijuwi kinachoendelea” anasema mwalimu mkuu
Naye Mwenyekiti wa kijiji hicho amesema ni kweli aliitwa na mwalimu mkuu wa shule hiyo na akawapa taarifa ya suala hilo lakini walichofanya waliondoka na mtoto pamoja na mtuhumiwa ambaye ndiye Baba mdogo wa mwanafunzi huyo wakaenda Hospital kuchukuwa vipimo na jibu wakapewa kuwa mwanafunzi huyo tayari kashatolewa Bikra.
Aidha amesema baada ya hapo waliongozana hadi kituo cha polisi kilichpo ndani ya kata yao na kuwapa taarifa pamoja na majibu ya vipimo na ndipo mkuu wa upelelezi katika kituo hicho akawambia waliachie jeshi la polisi kazi liweze kufanyia kazi.
“ni kweli niliitwa na mwalimu mkuu wa shule hiyo na akatupa taarifa ya suala hilo lakini tulichofanya wtuliondoka na mtoto pamoja na mtuhumiwa ambaye ndiye Baba mdogo wa mwanafunzi huyo tukaenda Hospital kuchukuwa vipimo na jibu tukapewa kuwa mwanafunzi huyo tayari kashatolewa Bikra ”
“baada ya hapo tuliongozana hadi kituo cha polisi kilichopo ndani ya kata yetu na kuwapa taarifa pamoja na majibu ya vipimo na ndipo mkuu wa upelelezi katika kituo hicho akatwambia tuliachie jeshi la polisi kazi”
“asaivi sijuwi kinachoendelea maana hata nikiuliza sipata majibu”
Redio mazingira fm tukifika katika kituo cha polisi hicho kilichotajwa lakini majibu tuliyopewa ni kuwa hawana taarifa ya mwanafunzi huyo wala taarifa yeyote kutoka uongozi wa kijiji hicho.
“Sisi hatuna taarifa ya huyo mwanafunzi mliyemtaja na hatujapokea taarifa yeyote kutoka kijiji hicho”
Ikatubidi tumtafute mama mzazi wa mwanafunzi huyo yeye amesema kuwa mwanaye amemusimulia hali ilivyo lakini alipowashirikisha watoto wake wa kiume Kaka zake na Mwanafunzi huyo walichosema ni kwamba waache tu maana mdogo wao yupo hai.
“amemusimulia hali ilivyo lakini nilipowashirikisha watoto wangu wa kiume ambao ni Kaka zake na huyo mwanangu wakaniambia mama achana na mambo hayo maana si mdogo wetu yupo hai kwamba waache tu maana mdogo wao yupo hai”
Taarifa zilipo ni kuwa mwanafunzi huyo amesafirishwa kupelekwa kwa mama yake mzazi kwa madai ya kuwa anaenda likizo lakini taariza tulizozipata kupitia chanzo chetu cha Habari ni kuwa mwanafunzi huyo mipango iliyopo ni kutorudi Shuleni.
Hata hivyo aliyeshiriki kumsafirisha kumpeleka kwa mama yake ni Yule Baba yake mdogo ambaye ndiye anayetuhumiwa kufanya kitendo hicho cha kikatili.

BADO TUNAENDELEA KUFATILIA HADI TUHAKIKISHE SUALA HILI TUNALIKAMILISHA.    

No comments:

Post a Comment