Wananchi wa mji wa Bunda wamempongeza Mkuu wa Wilaya kwa Hatua anazo zichukuwa. - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Saturday 23 December 2017

Wananchi wa mji wa Bunda wamempongeza Mkuu wa Wilaya kwa Hatua anazo zichukuwa.

Siku chache baada ya mkuu wa wilaya ya Bunda Mwl.Lydia Bupilipili kumuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Bunda Janeth Mayanja kuhakikisha ana wasimamia wahusika wote wa mipango miji ili waweze kuboresha na kusitisha uwanzishwaji wa masoko kila sehemu bila utaratibu,wananchi wa mji wa bunda wampogeza mkuu wa wilaya kwa hatua hiyo huku wakisema ofisi ya mipango miji imejisahau katika utekelezaji wa majuku yao.

Wakizungumza na mazingira fm kwa nyakati tofauti  baadhi ya wananchi hao wamesema kuwa wamefikia hatua ya kuanzisha masoko kiholela pasipo mpangilio kwa sababu hawaoni watu wakuwaelekeza juu ya upangiliaji wa mji hivyo kupelekea kukosesha mapato ndani halmashauri na serikali kiujumla kwa sababu ya watu wachache.


Hata hivyo wananchi hao wamesema kuwa pindi wataalam hao wataanza kuchukua hatua juu ya suala hilo wasiyafute masoko hao bali watoe utaatibu ili kama kuanza kutoa ushuru watu wapo tayari kufanya hivyo lakini siyo kuyafuta kabisa.

No comments:

Post a Comment