Vijana wilayani Bunda waaswa kuchapa kazi - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Sunday 24 December 2017

Vijana wilayani Bunda waaswa kuchapa kazi

Vijana katika Halmashauri ya Mji wa Bunda Mkoani Mara wameombwa kutambua kuwa wao ni nguvu kazi ya taifa siku zote, hivyo wanapaswa kufanya kazi kwa bidii bila kubagua kazi, ili kuweza kuleta maendeleo katika jamii na taifa kwa ujumla.

Ushauri huo umetolewa baadhi ya vijana wa mtaa wa wa bank wakati wakizungumza na redio mazingira hii leo.

James Juma pamoja na Naomi Kulwa Wamesema vijana wasipojituma kufanya kazi kwa bidii kauli ya kusema  vijana ni nguvu kazi ya taifa itabaki midomoni mwa watu bila vitendo vyovyote, hivyo ni wakati wakujituma ili kauli hiyo iwe kwa vitendo.


Katika hatua nyingine vijana hao wameiomba halmashauri ya mji wa Bunda, kuwajali vijana katika upande wa asilimia iliyotengwa na serikali ili kuweza kusaidia katika majukumu yao ya kujituma.   

No comments:

Post a Comment