Kijana mwenye umri wa miaka 24 amehukumiwa miaka 30 kwenda jela kwa kosa la kubaka Wilayani Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Friday 29 December 2017

Kijana mwenye umri wa miaka 24 amehukumiwa miaka 30 kwenda jela kwa kosa la kubaka Wilayani Bunda



Mahakama ya wilaya ya Bunda MkoaniMara , Desemba 27  2017 imemuhukumu kifungo cha miaka 30 jela Baraka saimon 24 mkazi wa kijiji cha Muranda kata ya Namuhura kwa kosa la kubaka  na kumpa mimba mwanafunzi  mwenye umri wa miaka 16 . 

Akisoma shtaka mbele ya hakimu mkaazi wa mahakama ya wilaya ya bunda Jacklin J. Rugemalira , mwendesha mashtaka upande wa jamhuri inspecta Masoud ameeleza mahakama kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo mnamo tarehe 19.oktoba.2017 saa za jioni.

Aidha amesema kuwa majira hayo mtuhumiwa alimbaka msachana huyo mwenye miaka 16 anaesoma katika shule moja ya sekondari.

Hata hivyo alipoulizwa kuhusu makosa hayo mshtakiwa amekiri kutenda kosa hilo na ndipo mheshimiwa hakimu amemhukumu kifungo hicho cha miaka 30 jela.

No comments:

Post a Comment