Mabwana Afya wanahitajika katika kijiji cha Sarama A wilaya ya Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Saturday 23 December 2017

Mabwana Afya wanahitajika katika kijiji cha Sarama A wilaya ya Bunda

Wakazi wa kitongoji cha Mumwaro kijiji cha Sarama A wilaya ya Bunda Mkoani  Mara wameiomba serikali kuwapelekea mabwana afya katika kitongoji hicho ili waweze kuondokana na uchafunzi wa mazingira kwa kujisaidia ovyo aja kubwa na ndogo katika vichaka.

Kauli hiyo imetolewa na wananchi wa kitongoji hicho walipokuwa wakizungumza na mazingira fm.

Wambura kigunya ambaye ni miongoni mwa wakazi wa kitongoji hicho amesema kuwa wakazi wa kitongoji hicho walio wengi hawana vyoo kitendo kinacho wapelekea kujisaidia vichakani bila kujua ni hatari kwa afya ya zao.

Amesema kuwa ni vizuri kama serikali ya kitongoji ita kuwa na utaratibu wa kupita kila mji na kukagua kama kunachoo ili kuweza kunusuru afya za wakazi wa kitongoji hicho pia kuepuka magojwa ya mlipuko kama vile kipindupindu na kuhara.

Hata hivyo  wameomba uongozi wa kitongoji hicho kuwachukulia hatua  za kisheria wale wote watakao bainika hawana choo katika miji yao ili iwe fundisho kwa wengine.


No comments:

Post a Comment