Hizi ni salamu tosha kwa wahalifu wilayani Bunda katika musimu huu wa sikukuu - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday 21 December 2017

Hizi ni salamu tosha kwa wahalifu wilayani Bunda katika musimu huu wa sikukuu

Jeshi la polisi wilayani Bunda Mkoani Mara limewahakikishia wananchi kuwa watasherekea sikukuu kwa amani na utulivu kwani wamejipanga kikamilrifu kukabiliana na wahalifu watakao taka kuchafua hali ya hewa katika musimu huu wa sikukuu.
Akizungumza kupitia kipindi cha Asubuhi leo kinachorushwa na kituo hiki Mkuu wa polisi Bunda kamanda Jeremiah Shila amesema wao kazi yao ni kuhakikisha wanalinda raia na mali zake hivyo katika musimu huu wa sikukuu wako makini sana katika suala la ulinzi kaika maeneo yote ya Wilaya ya Bunda lengo ni wananchi kuwa salama wakati wote.
OCD Shila amewatumia salama waharifu wote wanaopanga kuja kufanya uhalifu katika wilaya ya Bunda kuwa hata wasipoteze muda maana wao wamejiandaa kikamilifu.

OCD Shila pia amezungumzia suala la ulinzi na usalama Wilaya ya Bunda kufuati matukio mbalimbali kutokea hivi karibuni ikiwemo ya ukatili wa kijinsia yaliyojitokeza katika maeneo tofauti ndani ya wilaya ya Bunda na kusema kuwa wanayafanyia kazi matukio yote yaliojitokeza na kuomba wananchi kutochoka pindi polisi wanapotaka ushirikiano kutoka kwao.

No comments:

Post a Comment