Kibara sekondary waja na mikakati mipya yakufanikisha ndoto ya wanafunzi Wilayani Bunda - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Friday 29 December 2017

Kibara sekondary waja na mikakati mipya yakufanikisha ndoto ya wanafunzi Wilayani Bunda



KIKAO cha wazazi katika shule ya sekondari Kibara, iliyoko wilayani Bunda, mkoani Mara, kimepitisha maazimio kadhaa, ili shule hiyo iendelee kutoa elimu bora kwa wanafunzi na kufanya vizuri kitaaluma mara kwa mara.
Katika taarifa ya kikao hicho iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na mkurugenzi wa shule hiyo Mtamwega Mgaywa amesema kuwa kikao cha wazazi wa wanafuzi wanaosoma katika shule hiyo kimeketi desema 22 mwaka huu.
Amesema kuwa katika kikao hicho wazazi wamezungumzia changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo, ili kuzirekebisha na kuleta ufanisi zaidi, ili wanafunzi waendelee kupata elimu iliyo bora zaidi.
Mgaywa ameyataja baadhi ya maazimio ya wazazi hao kuwa ni pamoja na mtu yeyote kutokuifunga shule hiyo, bila kushirikisha wazazi wenye watoto na bodi ya shule na kwamba pia shule hiyo isiingiliwe na mtu yeyote, wanasiasa wala maslahi ya kisiasa, na badala yake ibaki na masuala ya elimu tu.
Ameyataja maazimio mengine kuwa ni migogoro yoyote ipelekwe kwenye bodi ya shule na ikishindikana ipelekwe kwenye vyombo vya sheria, ambapo jingine ni kama kuna madai yoyote yafuate utaratibu wa kazi na siyo vinginevyo.
Katika kikao hicho pia wazazi wameazimia mkuu wa shule hiyo afanye marekebisho ya ajira na azingatie mwenye sifa ya taaluma ya elimu, ikiwa ni pamoja na kuboresha uongozi wa shule na kwamba pia kitafanyika kikao cha wazazi na bodi hapo Januari 3, mwakani, ili kuweka mikakati mingine ya kimaendeleo zaidi.

No comments:

Post a Comment