Jeshi la Polisi Wilayani Bunda limetolea ufafanuzi tukio la ajali ya moto iliyotokea hivi karibuni - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Saturday 23 December 2017

Jeshi la Polisi Wilayani Bunda limetolea ufafanuzi tukio la ajali ya moto iliyotokea hivi karibuni

Imeelezwa kuwa ajali ya moto iliyotokea hivi karibuni katika Mtaa wa Sabasaba Kata ya Bunda Mjini Halmashauri ya mji wa Bunda Mkoani Mara na kusababisha kuungua kwa maduka mawili inasadikika kuwa chanzo cha ajali hiyo ni shoti ya umeme.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya Habari kuhusu tukio hilo Mkuu wa kituo cha polisi wilaya ya Bunda OCD Jeremiah Shila amesema kuwa kwa uchungzi wa awali wakishirikiana na Tanesco wameweza kubaini kuwa chanzo cha ajali hiyo ni shoti ya umeme iliyojitokeza katika moja ya maduka yaliyoungua.

Shila amesema bado wanaendelea kufanya uchunguzi zaidi ili waweze kubaini kisa kamili cha ajali hiyo.

Aidha Shila amesema kwa ushirikiano mzuri wa wananchi pamoja na Jeshi la polisi waliweza kuuzima moto huo licha ya kuwepo kwa changamoto ya gari la zima moto katika Wilaya Bunda.

Hata hivyo Shila ametoa wito kwa Wananchi wa wilaya ya Bunda kuwa wangalifu na umeme ikiwa ni pamoja na kuacha kupikia kwenye vibanda.


Ajali ya moto ilitokea mnamo tarehe 18.12.2017 majira ya saa tatu usiku katika mtaa wa sabasaba maeneo ya maduka ya wauza mitumba karibu na mlango wa kuingia soko kuu la mjini Bunda.

No comments:

Post a Comment