ZITO KABWE KUUNGURUMA KESHO UWANJA WA MKENDO MJINI MUSOMA. - Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Wednesday 7 June 2023

ZITO KABWE KUUNGURUMA KESHO UWANJA WA MKENDO MJINI MUSOMA.


Chama Cha ACT Wazalendo kesho tarehe 8 June 2023 kitafanya mkutano mkubwa wa siasa katika Viwanja vya shule ya msingi Mkendo Manispaa ya Musoma Mkoani Mara.

Hii ikiwa ni mwendelezo wa mikutano yake tangu ilivyozindua mikutano hiyo mwezi February 2023 Jijini Dar es Salaam baada ya kuruhusiwa mikutano ya kisiasa.

Akizungumza na Radio Mazingira Fm kupitia kipindi Cha Asubuhi leo, Mratibu wa Mikutano na Afisa wa ACT – Wazalendo makao makuu, Ndugu Mussa Bakari ‘ Tembo’ amesema tangu kuondolewa zuio la mikutano ya hadhara chama kimefanya mikutano katika Mikoa 9 awamu ya kwanza na sasa katika awamu ya pili watafanya katika Mikoa 10.

No comments:

Post a Comment